Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na wananchi wa Urambo wana imani na Wizara hii inafanya kazi kubwa, lakini kwa leo naiomba Serikali itoe kauli hapa. Lini maji haya yanafika Urambo kutokea Tabora ambapo yameshafika kutoka Lake Victoria?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la ngongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema lini mradi utaanza kutekelezwa, kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha, mradi utaanza kutekelezwa. (Makofi)

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 2

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Serikali ilianza mpango wa kulipa fidia wananchi wa maeneo yaliyozunguka Mradi wa Mto Ruvuma, sasa nataka kujua kwa nini Serikali inakwama kuendeleza mradi huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli fidia ilishaanza kulipwa na itaendelea kumaliziwa ndani ya mwaka huu wa fedha, lakini mradi huu wa Mto Ruvuma ni katika ile miradi yetu ya kimkakati ndani ya Wizara kuona kwamba vinakuwa nyanzo vya kudumu kwa kutoa huduma ya maji kwa wananchi.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 3

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; hali ya upatikanaji maji Wilaya ya Mkinga kwa sasa ni mbaya sana. Hivi ninavyozungumza mabwawa takribani matano yamekauka, tumeanza kuona dalili za ugonjwa wa homa ya matumbo. Sasa Wizara ilituma wataalam kufanya usanifu wa mradi mkubwa wa kutoa maji Mto Zigi kwenda mpaka Horohoro ambapo kazi hiyo inakamilika kesho. (Makofi)

Je, Serikali iko tayari kwa udharura huu kuhakikisha inaharakisha mchakato wa kupata wakandarasi, ili mradi ule uanze kushughulikiwa haraka iwezekanavyo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kitandula, Mbunge wa Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunafahamu maji ni uhai na sisi kama Wizara ya Maji hatupendi kuwa kikwazo na kusababisha milipuko ya magonjwa. Kwa kutambua hilo kama Wizara tunamshukuru Mheshimiwa Rais aliongoza dua na sasa hivi mvua zimeanza kunyesha vizuri, mabwawa yaliyokauka tunayatarajia yarudi katika hali yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika usanifu huu unaoendelea ambao tunautarajia ukamilike kesho, tutaharakisha kuona kwamba lile bwawa ambalo linafanyiwa usanifu na maeneo yale ya Mkinga yote tunakwenda kuyafanyia kazi kwa haraka. Ninawaagiza ile timu iliyotumwa kule na Mheshimiwa Waziri ifanye kadri ya maagizo ya Mheshimiwa Waziri yaliyopo ili kuona tunaharakisha jambo hili. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Manyoni Mashariki tuna mradi mkubwa wa shilingi bilioni 10 unaojulikana kwa jina la Kintinku-Lusilile. Kwanza naishukuru Serikali mpaka sasa hivi tayari chanzo cha maji kimepatikana. Lakini ningependa kusikia majibu ya Serikali ni lini sasa mkandarasi wa kusambaza maji, katika mradi huo katika Kata za Kintinku, Maweni na Makutupora ataanza kazi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pius Chaya; ni kweli mradi huu una vijiji 11 na tayari vijiji vitatu vimeshaanza kufanyiwa kazi na wiki ijayo tunatarajia kusaini mkataba wa kukamilisha vijiji nane vilivyobaki na tayari tumetenga fedha zaidi ya shilingi bilioni 3.3 ili mradi huu uweze kuendelea katika utekelezaji wake. (Makofi)

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 5

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza.

Mji wa Mpanda ni kati ya miji 28 ambayo inatakiwa kupewa mradi wa maji; ni lini mradi huu utaletwa Mji wa Mpanda? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapufi kutoka Mpanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi hii ya miji 28 tutarajie itaanza ndani ya mwezi huu wa pili au wa tatu kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha.

Name

Humphrey Herson Polepole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 6

MHE. HUMPHREY H. POLEPOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za Kitafiti zinasema kila mwaka tani milioni tatu za udongo zinaingia katika Ziwa Victoria na kulipunguzia Ziwa hilo kina cha maji. Serikali ina mpango gani na iko katika hatua ipi ya kutekeleza National Water Grid au mtandao wa maji wa kitaifa kutoka Kusini, Kaskazini, Magharibi ili kuweza kupunguza pressure katika Ziwa Victoria? Nakushukuru sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Polepole kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna hii changamoto ya matope kuingia katika vyanzo vyetu vya maji na sisi kama Wizara tuna ofisi zetu za mabonde zinazoshughulika na kazi hizi na tayari Mheshimiwa Waziri amewaagiza. Hivyo, tayari hili linafanyiwa kazi kuona kwamba tunaendelea kutunza na kuvilinda vyanzo vyetu vya maji. (Makofi)

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: - (a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Supplementary Question 7

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba nataka nielewe sisi kule kwetu Mtwara nimechimbiwa visima vitatu katika Jimbo langu, lakini takriban mpaka sasa hivi karibu miezi minne inakimbilia na mvua zinaanza kunyesha na visima vile tayari vimeshaanza kuziba.

Ni lini sasa visima vile vitamaliziwa kwa taratibu zingine za upatikanaji wa maji? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamshukuru Mwenyezi Mungu; Mheshimiwa Rais alitupatia fedha na visima vimechimbwa, kinachofuata ni mtandao wa usambazaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatoa agizo kwa Mameneja wa Mtwara wafanye kazi haraka iwezekanavyo ndani ya mwezi mmoja, waweze kuona kwamba utaratibu wa mwendelezo wa visima hivi inaweza kufanyika. (Makofi)