Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 32 2022-02-04

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

(a) Je, ni lini Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria Wilaya ya Urambo utaanza ili kutatua tatizo la maji katika Wilaya hiyo?

(b) Je, ni lini Serikali itachimba mabwawa katika Kata za Uyumbu na Kalemela hasa ikizingatiwa kuwa maombi yalishawasilishwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa huduma ya maji katika Wilaya ya Urambo ni wastani wa asilimia 40. Katika kuboresha huduma hiyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 inatekeleza miradi ya Itibulanda na upanuzi wa mradi kutoka Itibulanda kwenda Nsenga. Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 50,000, vituo 13 vya kuchotea maji na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 17.6. Miradi hiyo itaongeza uzalishaji maji wa lita 32,000 kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuboresha huduma ya maji katika Kata za Uyumbu na Muungano, Serikali imepanga kujenga mabwawa mawili ya Kilemela kata ya Muungano na Izimbili kata ya Uyumbu. Mabwawa hayo yatahudumia jumla ya vijiji vya 22 na mkandarasi wa ujenzi wa bwawa la Kilemela atapatikana mwezi Aprili, 2022 Kwa upande wa bwawa la Izimbili kazi ya usanifu inaendelea na itakamilika mwezi Juni, 2022. Ujenzi wa mabwawa hayo utafanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Aidha, Mji wa Wilaya ya Urambo unatarajiwa kupata huduma ya maji kupitia Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji 28 ambapo chanzo cha maji kitakachotumika ni Ziwa Victoria. Taratibu za upatikanaji wa wakandarasi zimekamilika mwezi Desemba, 2021 hivyo utekelezaji utaanza ndani ya mwaka wa fedha 2021/2022.