Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa maboma fedha nyingi zimeonekana zimeshindwa kuyakamilisha maboma yaani kiwango cha shilingi milioni 50 zinakwenda kwenye vijiji lakini maboma hayaishi.

Je, Serikali imefanya tathmini ya kina kujua kwamba level ya maboma iliyofikiwa kwa nguvu za wananchi inahitaji fedha kiasi gani ili kumaliza maboma?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ninaomba kumuuliza Waziri ni lini sasa Serikali itapeleka watumishi katika zahanati ambazo zimetengewa fedha na kukamilika ili kuhakikisha wananchi wetu wote wanapata huduma katika zahanati husika katika maeneo husika? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Kingu kwa uchapakazi wake mzuri kwa kuwasemea wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi na kwa kweli Serikali tutaendelea kumpa ushirikiano kuhakikisha wananchi wanapata miradi hiyo ya maendeleo kwa ustawi wa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi ambazo zimepelekwa kwenye ukamilishaji wa maboma ya zahanati, kila boma ambalo limefikia hatua ya lenta linatengewa shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji na tathmini ilifanyika kwa sababu ramani zile zilitolewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na BOQ zake zilionesha jengo likijengwa mpaka hatua ya lenta likipewa shilingi milioni 50 jengo lile linakamilishwa bila changamoto yoyote na ndiyo maana katika maboma 555 yaliyopelekewa takribani shilingi 27,750,000,000 mwaka wa fedha uliopita zaidi ya asilimia 85 ya maboma yamekamilika, yameanza kusajiliwa kwa ajili ya kuanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo tathmini ilifanyika, lakini kuna variation za kimazingira za hapa na pale ambazo nazo huwa tunazizingatia na kama inajitokeza variation kama hiyo basi tunaona namna nzuri ya kukamilisha ujenzi wa zahanati hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili ujenzi wa zahanati na vituo vya afya kwa ujumla wake unakwenda sambamba na mpango mkakati wa kuajiri watumishi ili zahanati na vituo vianze kutoa huduma na tayari Serikali tumefanya tathmini ifikapo Juni, 2022 tutakuwa na vituo 1,073 ambavyo vitakuwa vimekamlika na tumeshafanya tathmini ya mahitaji ya vifaa tiba, lakini pia na watumishi na kwa kadri ya bajeti yetu tutaendelea kupeleka watumishi ili vituo vile vianze kutoa huduma na kupunguza upungufu wa watumishi katika maeneo hayo, ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime inaelemewa kwa kupokea wagonjwa wengi kutoka nje ya mji wa Tarime mathalani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Serengeti, Rorya na hata wakati mwingine kutoka nchi jirani ya Kenya.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kukamilisha kituo cha afya cha Kenyamanyori pamoja na zahanati ya Nyandoto ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi ili walau kupunguza pressure ambayo inapelekea msongamano katika hospitali ya Mji wa Tarime?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kuhakikisha tunajenga zahanati na vituo vya afya ili kupunguza kwanza umbali wa wananchi kupata huduma, lakini pili kupunguza msongamano kwenye hospitali za Wilaya kama ilivyo katika hospitali ya Wilaya ya Tarime.

Kwa hivyo suala hilo ni la msingi na mipango hiyo tayari imewekwa, wito ambao nautoa kwa Halmashauri ya Tarime ni kutoa kufanya tathmini ya mahitaji ya fedha zinazotakiwa kukamilisha kituo cha afya na zahanati, pili kutenga kupitia mapato ya ndani, lakini pia Serikali Kuu tunaendelea kuangalia fursa ya kupeleka fedha ili kukamilisha zahanati hizo, ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 3

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona changamoto ya Jimbo la Singida ziko sambamba kabisa na changamoto ambazo zinaikabili wilaya ya Chunya kwenye umaliziaji wa maboma; kuna boma lililojengwa kwa nguvu ya wananchi kwenye kata ya Ifumbo lina zaidi takribani miaka minne halijakamilika.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha ili ukamilishaji wa boma hili kwenye kata ya Ifumbo iweze kukamilika ilihali ukijua kata hii iko mbali sana na Makao Makuu ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu la Mheshimiwa Kasaka, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimwia Mwenyekiti, katika ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati tumeainisha maeneo ya kimkakati, na tuliwaomba Waheshimiwa Wabunge kuwasilisha vipaumbele. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge, kama Kituo cha Afya katika Kata ya Ifuko ni kipaumbele basi tupate taarifa hiyo rasmi ili tuweze kuweka mpango wa kuhakikisha kwamba tunakamilisha ili wananchi wapate huduma. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 4

MHE VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ili na mimi niulize swali moja la nyongeza.

Je, Serikali inaweza kutuweka katika orodha vijiji vyetu vya Ulamboni, Kilangalanga, Chengena, Luhangano na Mhangazi vyenye maboma ambayo hayajaisha ili waweze kupata hizo shilingi milioni 50 waweze kumalizia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya kote nchini unafanywa kwa fedha za Serikali Kuu pamoja na fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri. Kwa hiyo, kuna vile vituo ambavyo vitakamilishwa kwa fedha za Serikali Kuu na hivyo tumeviainisha, lakini ukitokea uhitaji tutaainisha pia vikiwemo hivi vituo vya Kilangalanga na vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nitoe wito kwamba ujenzi wa zahanati hizi ni lazima pia Halmashauri kupiti mapato yake ya ndani, kupitia asilimia 40 ya fedha za miradi ya maendeleo au asilimia 60 watenge fedha kwa ajili ya kukamilisha baadhi ya maboma, wakati Serikali Kuu pia inatafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Kawawa kwamba tumelichukua hilo na tutawasiliana kuona yapi yakamilishwe kwa mapato ya ndani na yapi tutafute fedha kutoka Serikali Kuu.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 5

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo kwa Mheshimiwa Waziri.

Je, Serikali ina mpango gani wa kumailizia Kituo cha Afya cha Gidas ambacho kinahudumia si tu wananchi wa Kata ya Gidas ila pamoja na wananchi wa mipakani mwa Kondoa? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati njema wiki iliyopita tulikuwa kwenye ziara jimboni kwake na tulipita katika maeneo haya ikiwepo katika Kituo cha Afya cha Gidas.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie, kama tulivyokubaliana kwamba kituo kile ni cha kimkakati, tutakwenda kutafuta fedha ili kukikamilisha ili tuweze kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 6

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Mji wa Mafinga nadhani ndiyo hospitali inayohudumia Halmashauri nyingi kuliko hospitali yoyote hapa nchini. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia zaidi ya Halmashauri tano ikiwepo ya Mlimba ambayo iko Mkoa wa Morogoro. Sasa kutokana na unyeti huo, na kwamba iko kando ya barabara kuu.

Je, Seikali iko tayari kuleta watumishi katika mpango wa dharura?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Mafinga ni kweli iko barabarani na inahudumia wananchi wengi; na hospitali zote ambazo ziko kimkakati tunaziainisha na kuziwekea mpango, kwanza wa kupeleka vifaa tiba, lakini pia kuboresha upatikanaji wa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie kwamba tutakwenda kwa utaratibu wa kawaida wa kupata watumishi kwa ajili ya hospitali ile badala ya utaratibu wa dharura, kwa sababu utaratibu wa watumishi unapatikana kupitia vibali maalum; laini tutaaipa kipaumbele Hosptali ya Mji wa Mafinga.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Je ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi katika ujenzi wa zahanati za Nsengoni, Gaisosya, Kikatiti na Samaria? Wananchi wamehangaika kuzijenga zahanati hizi kwa miaka mingi lakini hawaoni support ya Serikali.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu kweli swali la msingi, mwaka wa fedha uliopita zaidi ya shilingi 27,750,000,000 zilipelekwa ili kukamilisha maboba 555, lakini katika mwaka wa fedha huu wa 2021/2022 zaidi ya shilingi bilioni 28.2 pia zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha maboma 564 ya zahanati.