Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 28 2022-02-04

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza maboma ya Zahanati ya Ufana, Kinyampembe, Mpeti, Misake, Mlandala, Kaugeri na Mtavira ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika Jimbo la Singida Magharibi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kujenga vituo vya kutolea huduma za afya kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuboresha utoaji wa huduma za afya ya msingi kwa wananchi ikiwemo ukamilishaji wa maboma ya zahanati. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 28.2 za ruzuku kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 564 katika Halmashauri zote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Disemba, 2021 tayari Serikali imepeleka shilingi bilioni 15.4 katika Halmashauri nchini kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti iliyopangwa ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 200 kimepelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kutekeleza ukamilishaji wa maboma ya zahanati nne za Ufana, Kinyampembe, Misule na Makotea. Aidha, Halmashauri kutumia mapato ya ndani imetenga shilingi milioni 50 kukamilisha boma la zahanati ya Kaugeri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka mpango wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya zahanati yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi. Aidha, Serikali inazielekeza Halmashauri zote nchini kuendelea kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati hizo ili ziweze kutoa huduma tarajiwa kwa wananchi, ahsante.