Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawatambua watoto wenye ulemavu ambao wanaishi kwenye mazingira magumu ili kuwasaidia kwa matibabu na kimaisha?

Supplementary Question 1

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri maana yamekuwa safi tofauti na penalty ya Simba ya jana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba hawa watoto wenye walemavu mara nyingi huwa wanarandishwa randishwa mitaani na unaweza ukaja ukamkuta mtoto anarandishwa mtaani na watoto wenziwe maana yake mpaka hawa wengine wanakosa zile haki za watoto.

Sasa ndiyo maana nikauliza ni lini kwa sababu tunaona bado wako mtaani wanarandishwa ni lini hasa hatua stahiki za ukweli ukweli zitachukuliwa ili kupunguza lini wimbi? Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili wazee wengi huwa wanashindwa hizo huduma tunazoambiwa wanapewa wanashindwa kuwapelekwa watoto hawa kwenda kupata huduma, wengine wanahitaji kwenda kupelekwa kwenye mashine kufanyishwa mazoezi, lakini wengine wanahitaji mambo tofauti tofauti, lakini ingawa limejibiwa hapa lakini tunaona kwamba ni bado hicho kitu kinaendelea.

Kwa hiyo niiulize Serikali ni lini hili jambo la watoto kupatiwa hizi huduma ambazo wanahitaji wakati mwingine zinatolewa kwa pesa watapata bure ili wale wazee nao waweze kupata faraja? Nashukuru.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ali King, la kwanza akiuliza kwamba hawa watoto wamekuwa wakirandishwa randishwa mitaani kwa maana ya kuzururishwa.

Ni lini hatua stahiki zitachukuliwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Serikali wamekwisha kuanza kuchukua hatua hasa pale matendo kama hayo yanapofanyika mitaani na kwa kuzingatia mwongozo huo ambao umetolewa ambao ni Mwongozo wa Taifa Utambuzi wa Mapema Afua Stahiki za Watoto wa Watu Wenye Ulemavu. Lakini pia kwa mujibu wa sheria tulizonazo na moja ya sheria ni hizo za utekelezaji wa sheria za watoto ambapo watoto wana haki na stahili zao zimeainishwa kwa mujibu wa sheria.

Kwa hiyo, pale inapobainika kwamba kuna changamoto kama hizo kwenye mitaa yetu hatua zimekuwa zikichukuliwa kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa sababu zimeainishwa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2019. Kwa hiyo, hatua tayari tumekwisha kuanza kuchukua.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri inatosha ameshakuelewa.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu huduma; tayari Serikali imekwisha kutambua watoto zaidi ya 76,247 na ilibaini watoto wenye changamoto hizo ni 42,373 na hivyo tayari umekwisha kuingia kwenye mpango kupitia rejista ambayo iko ya utambuzi chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Makundi Maalum, lakini sambamba na hilo pia Ofisi ya Rais, TAMISEMI inaendelea na shughuli hiyo ya usimamizi na uratibu wa masuala ya ulinzi na usalama wa Watoto, ahsante.