Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR Aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Vituo vya Afya vya Kharumwa na Nyang’hwale?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyonge kwanza niipongeze Serikali kwa kutupatia watumishi 20 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 watumishi watatu kituo cha afya Karumwa na wanne kituo cha afya Nyang’ahwale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023 kutokana na upungufu uliopo katika vituo vyetu vya Nyang’gwale ambavyo sasa hivi wilaya hiyo imekuwa na mfumuko mkubwa wa madini na watu wengi wamejazana katika wilaya hiyo huduma bado inaitajika sana kwenye kituo cha afya kama vile wilaya Je, Serikali iko tayari kutuongezea watumishi kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita ya mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha nyingi katika sekta ya afya na kuweza kukamilisha zahanat zaidi ya 10 ambazo tunatarajia kuzifungua hivi karibuni. Je, Serikali imejipanga vipi kutupatia vifaa tiba na watumishi ili tuweze kuanzisha huduma katika zahanati hizo 10.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nassor Hussein Amar Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee pongezi zake nyingi kwa Serikali hii inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo imefanyika katika sekta ya afya. Lakini nimuhakikishie katika mwaka huu wa fedha 2021/2022 kuna vibali vya ajira ambavyo vitatolewa ili kuajiri watumishi kwenda kupunguza upungufu wa watumishi katika vituo vyetu vya afya kote nchini vikiwepo vituo vya afya katika halmashauri na Jimbo hili la Nyang’hwale. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Jimbo la Nyang’hwale katika vituo hivi vitapewa kipaumbele katika ajira inayokuja ili kuhakikisha tunapeleka watumishi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili ni kweli kwamba tumeendelea kujenga vituo vingi katika mamlaka ya Serikali za Mitaa na Serikali imeshafanya tathimini tunajumla ya vitu 1073 ambavyo tunatarajia ifikapo Juni mwaka huu vitakuwa vimekamilika na vitahitaji vifaa tiba, vitahitaji watumishi na tathimini imeshafanyika na maandalizi ya kupata vifaa tiba hivyo na watumishi imeshafanyika kwa hiyo iliyobakia ni suala la utekelezaji. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba vituo vyetu ambavyo vinaendelea kujengwa tayari tathimini inajulikana na kazi yakupeleka watumishi na vifaa tiba itakwenda kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR Aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Vituo vya Afya vya Kharumwa na Nyang’hwale?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais wetu kwa fedha tulizopata kwa kujenga vituo vya afya Pamoja na kukarabati kituo cha kule Kirua Vunjo na Marangu headquarter. Nina swali kuhusu kituo ambacho tumeahidiwa pale OPD Himo mji mdogo wa Himo. Kituo hiki kinahudumia watu wengi sana watu zaidi ya 36 elfu lakini bahati mbaya hakina majengo ya upasuaji, mahabara na Mochwari na tulipoahidiwa hili jambo na Mheshimiwa Naibu Waziri wa afya wakati wa kampeni tulijua kwamba tutafanyika na imefanyika lakini haya majengo hayapo. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, ni lini tutapata fedha kwa kujenga majengo haya ili kituo hiki sasa kiweze kutumika na kutoa huduma zote zinazostahili kwa kituo cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei Mbunge wa jimbo la Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunavituo vingi nchini vikiwepo vituo vya Jimbo Vunjo ambavyo kwanza vinamiundombinu michache kulinganisha na huhitaji wa vituo vya afya ikiwemo majengo kama mahabara majengo ya upasuaji lakini pia upungufu wa mawodi. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo cha afya cha OPD himo ni miongoni mwa vituo ambavyo tumeviahinisha na tumeviwekea mpango kazi wa kutafuta fedha ili kwenda kujenga majengo hayo ambayo yatavifanya vikamilike kuwa vituo vya afya na hatimaye viweze kutoa huduma zile ambazo zinatarajiwa. Kwa hiyo, tunatafuta fedha Mheshimiwa Mbunge na niwahakikishie kwamba fedha ikipatikana tutawapa kipaumbele kitu cha afya cha OPD Himo.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR Aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Vituo vya Afya vya Kharumwa na Nyang’hwale?

Supplementary Question 3

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hali ilivyo maeneo ya Jimbo la Nyang’hwale inafanana na kabisa na hali ilivyo kwenye Jimbo la Sumve ambalo lina Kituo cha Afya cha Nyambiti ambacho kilibadilishwa kilikuwa zahanati na kituo hicho cha afya kina hudumia kata 13 za Jimbo la Sumve ambazo zina wakazi zaidi ya laki mbili na kituo kile hakina majengo kama ya upasuaji mahabara na majengo ya muhimu ambayo yangesaidia katika kutoa huduma stahiki ya afya kwa watu wale. Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha watu wa Jimbo la Sumve katika kituo cha afya cha nyambiti na wenyewe wanapata huduma nzuri kama ilivyo katika vituo vingine vya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali Mageni Mbunge wa Jimbo la Sumve kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla katika halmashauri zetu na katika majimbo yetu tuna vituo vya afya ambavyo vina majengo pungufu kama nilivyotangulia kujibu katika jibu langu lililopita na mpango wa Serikali ni kuhakikisha standard ya vituo vya afya inafikiwa kwa maana ya kuwa na majengo yale yote ya muhimu yanayofanya kituo kile kiwe na hadhi ya kuwa kituo cha afya. Kwa hiyo, kuwepo kituo hiki cha afya cha Nyambiti katika jimbo hili Mheshimiwa Mbunge naomba nimuhakikishie kwamba tutafanya tathimini pia kuona umetupa taarifa kwamba hakuna majengo ya upasuaji na mahabara na tunajua ni muhimu na yanahudumia zaidi ya kata 13 ni moja ya kituo cha afya cha kimkakati na ninajua ulikihainisha kwa hiyo tukitafuta fedha tutahakikisha tunaipa kipaumbele kujenga majengo hayo ili wananchi wale wote wapate huduma bora za kituo cha afya.