Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2022-02-03

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR Aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika Vituo vya Afya vya Kharumwa na Nyang’hwale?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nassor Hussein Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha upatikanaji wa watumishi wa kada za Afya katika Vituo vya kutolea huduma za Afya ili kuendana na upanuzi wa miundombinu ya Afya ya Msingi nchini. Katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 Serikali iliajiri watumishi 2,726 wa kada mbalimbali za Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika ajira hizo za Serikali, Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale ilipangiwa watumishi 20 ambapo Kituo cha Afya Kharumwa kilipata watumishi 3 na Kituo cha Afya Nyang’hwale kilipata watumishi 4.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri na kugawa watumishi kwenye Halmashauri na Vituo vya kutolea huduma za Afya kadri ya upatikanaji wa vibali vya ajira na fedha ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.