Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO Aliuliza: - Je, lini Serikali itawaunganishia umeme wa REA wananchi wa Vijiji vilivyopo katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki ambazo hazina umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili niliuliza kwa sababu kuna kata nyingi sana kule ambazo hazijapata umeme hususani Kata ya Uwilo kuna vijiji kama viwili vile Lukulu Skimosoni na kule Maruhango pia kuna vijiji maruhango kwenye hakuna umeme je, niulize ni lini hasa vijiji hivyo vitapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Pallangyo na nimshukuru kwa ufuatiliaji na uvumilivu kwa sababu jimbo lake ni moja ya majimbo ambayo mkandarasi alichelewa kupatikana kwa sababu ya taratibu ya kimanunuzi. Lakini kama nilivyosema kwenye swali na jibu la msingi ni kwamba kufikia Disemba mwaka huu kwa mujibu wa mkataba kata zote ambazo hazina umeme ambazo ni vijiji kwakwe ni vijiji 12 ndiyo havina umeme vitakuwa vimepatiwa umeme kwa kadri ya mkataba tuliokuwanao.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO Aliuliza: - Je, lini Serikali itawaunganishia umeme wa REA wananchi wa Vijiji vilivyopo katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki ambazo hazina umeme?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilini Serikali itajenga substation ya kule Mkuranga sambamba na kuweka transformer ya NVA 90 pale katika substation ya Mbagala ili kuondoa tatizo la ukatikaji wa umeme mara kwa mara katika jimbo la Mbagala?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, jimbo la Mbagala linalo substation ndogo kama alivyosema ambayo ina transformer yenye uwezo wa AVA 50 NA substation hiyo inapeleka umeme mpaka maeneo ya mkulanga na kwa bahati nzuri ambayo inakuwa mbaya kwa upande mwingine. Eneo la Mkulanga limekuwa na viwanda vingi sana na hivyo linachukua umeme mwingi sana kutoka eneo la Mbagala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshaanza upembuzi wa kujenga kituo cha kupoza umeme eneo la Mkulanga ambacho kitakuwa kina zaidi ya Megawatt 100 lakini taratibu za kukamilisha ununuzi wa transformer ya AVA 90 itakayokuja kufungwa pale Mbagala zinakamilika na tunaamini kabla yam waka huu kuisha kituo cha Mbagala kitakuwa kimeongezewa uwezo wakati kule Mkulanga substation ikiwa inapatikana fedha kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO Aliuliza: - Je, lini Serikali itawaunganishia umeme wa REA wananchi wa Vijiji vilivyopo katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki ambazo hazina umeme?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL J. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na sinto fahamu kubwa juu ya kiwango gani kitozwe kwa wananchi ili kuweza kuvutiwa umeme kwenye maeneo mbalimbali wakiwemo wananchi wa eneo la Nasio Wilaya Ukerewe. Nilitakakujua ni vigezo gani vinavyotumika kujua ni kiwango gani cha pesa kinatakiwa kulipwa na mwananchi ili aweze kuvutiwa umeme kwenye eneo lake la nyumba.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Mkundi kwa swali lake nzuri Mbunge wa Ukerewe ambaye pia amekuwa akifuatilia sana mambo ya umeme katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakumbuka tulikuwa tume standardize gharama za upatikanaji wa umeme lakini baadaye tulimuomba Mheshimiwa Rais atukubalie tufanye marekebisho katika baadhi ya maeneo ili kuweza kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumerudi kwenye vile viwango ambavyo tulikuwa tunavitumia hapo awali ambapo maeneo ya mijini yanapata umeme kwa gharama ambazo wenzetu wa EWURA ndiyo wa simamizi wa gharama wameziweka zinaanzia laki tatu na kuendelea. Lakini maeneo ya vijijini yanapata umeme kwa gharama ya shilingi elfu saba kwa line ya njia moja na gharama nyingine zile za kawaida kwa njia tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwango na vigezo ambavyo tunavitumia viko katika sheria ya mipango miji ile ndiyo inayosema hapa ni jiji hapa ni mji hapa ni Kijiji na hapa ni nini. Kwa hiyo, kwa kutumia sheria hiyo ambayo inatumiwa na wenzetu wa TAMISEMI na watu wa ardhi tunaitumia hiyo sasa ku-decide kwamba hapa itakuwa 27 hapa itakuwa zile gharama za mijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajipanga kuendelea kutoa elimu kubwa Zaidi ili wananchi waweze kuelewa kwamba kiwango gani kinatozwa wapi na kwa sababu zipi kwa mfumo huo niliousema kwa hapo.