Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 17 2022-02-03

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO Aliuliza: -

Je, lini Serikali itawaunganishia umeme wa REA wananchi wa Vijiji vilivyopo katika Kata za Jimbo la Arumeru Mashariki ambazo hazina umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Arumeru Mashariki lina jumla ya Kata 26 na vijiji 90. Ni vijiji 12 tu ambavyo havina umeme na sasa vinapatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotekelezwa katika Jimbo la Arumeru Mashariki. Kazi zinazofanyika sasa ni usanifu wa kina, upimaji, uandaaji wa michoro na manunuzi ya vifaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi huu unahusisha ujenzi wa njia za umeme ya msongo kilovoti 33 zenye urefu wa kilomita 40.30; kilomita 12 ya njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4; ufungwaji transfoma 12 za KVA 50; pamoja na kuunganisha wateja wa awali 264. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 2.071 na utekelezaji wake unatarajiwa kukamilika Mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine Serikali imefanya uhakiki na kuainisha uwepo wa vitongoji takriban 37,610 visivyokuwa na umeme Tanzania Bara na inakadiriwa kuwa shilingi trillion 7 zitahitajika ili kukamilisha mahitaji ya umeme katika vitongoji hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekwishaanza utekelezaji wa miradi ya ujazilizi unaolenga kufikisha umeme katika vitongoji vyote Tanzania Bara awamu kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ikiwa ni pamoja na Vitongoji vya Jimbo la Arumeru Mashariki.