Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kutoa ajira rasmi na zisizo rasmi kupitia tasnia ya Sanaa?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa ni jukumu la Serikali kukuza, kuibua na kuendeleza sanaa nchini, tunatambua kuna vijana wengi sana nchini wana vipaji, lakini wanashindwa kuvitumia vipaji vyao kulingana na mazingira magumu yaliyopo ya kufanya vipaji hivyo na huenda vipaji hivyo vingeweza kuwapatia ajira.

Je, ni nini mpango wa Serikali wa kuibua, kuendeleza na kusimamia vipaji hivi vya vijana walioko katika nchi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunatambua kwamba kuna taasisi na watu binafsi wanaofanya matamasha ya kuibua vipaji: -

Je, ni nini kauli ya Serikali katika kuwaidia hizi taasisi au watu binafsi wanaofanya matamasha na jitihada za kusaidia kuinua vipaji Tanzania?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Sylvia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe taarifa tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na maswali ya msingi ambayo yalijieleka moja kwa moja kwenye swali la kwanza ambalo limeulizwa kama swali la nyongeza, Wizara yetu inajipanga vyema kutafuta vijana wenye vipaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwataarifu Waheshimiwa Wabunge kwamba mimi na wasaidizi wangu tumejipanga kupita katika kila mtaa ili kuweza kutafuta vijana wenye vipaji mbalimbali. Pia, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, Serikali imejipanga vizuri; na Mheshimiwa Rais tayari ameshaanzisha mfuko maalum ambao utawasaidia vijana wenye vipaji.

Kwa hiyo, tutapita kila mtaa, kila kijiji, kila wilaya, kila halmashauri katika kila mkoa kuhakikisha kwamba tunawasaka vijana wenye vipaji na kuweza kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili linalozungumzia matamasha yanayofanywa na baadhi ya watu na taasisi, sisi kama Wizara hatutakuwa na jambo dogo. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Wizara haitakuwa na jambo dogo, kila jambo litakuwa na uzito wake. Kwa hiyo tutashiriki katika kila kitu kinachofanyika kinachohusu utamaduni, sanaa na michezo ambacho wenzetu katika taasisi mbalimbali wamekuwa wakitusaidia Serikali.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kutoa ajira rasmi na zisizo rasmi kupitia tasnia ya Sanaa?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa sanaa imekuwa chanzo kikuu cha ajira kwa vijana wetu, je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kutumia vyuo vyetu vya VETA kama vituo vya kuibua na kuendeleza vipaji vya sanaa kwa vijana wetu?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu ya swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Mbunge wa Mikumi, mchapa kazi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ushauri mzuri aioutoa kuhusu matumizi ya vyuo vya VETA, lakini sisi kama Serikali tunakwenda mbele zaidi. Tunategemea kutumia baadhi ya shule tulizonazo kutengeneza academy mbalimbali. Tutatumia shule aidi ya 56 ambazo Serikali imejipanga kuzitumia kwa ajili ya kuendeleza na kukuza vipaji katika maeneo hayo.