Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU Aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha kipengele cha “moving expenses” kilichotolewa ili watumishi walipwe fedha za nauli wakati wakisubiri mafao mengine?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nilikuwa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza je, Serikali iko tayari sasa kuweka utaratibu wa muda maalum kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hizo moving expenses zinalipwa ili kuondoa usumbufu kwa watumishi wa umma?

Lakini swali langu la pili je, ni lini sasa Serikali pia itafanya marekebisho kwa yale madaraja ya watumishi wa umma yaliyofutwa mwaka 2016 na 2017. Hasa katika Manispaa yangu ya Iringa wapo watumishi zaidi ya 300 ambao hawajafanyiwa marekebisho pamoja na kazi nzuri ambayo imefanywa na Serikali ya kupandisha madaraja. Ni lini itafanya kazi hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na pia tumeshaleta sana hili ombi mara nyingi sana kwa Waziri lakini halijafanyiwa kazi, tunaomba commitment ya Serikali? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la kwanza kama nilivyosema kwenye majibu ya msingi. Waajiri wote wanatakiwa kuhakikisha wanatekeleza matakwa ya Kanuni za Kudumu za Kudumu za Utumishi wa Umma na tayari Kanuni hizo zipo kwamba ni Mtumishi yoyote anapokoma utumishi wake wa umma au mtumishi pale anapohama anastahili kulipwa moving expenses.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nitumie fursa hii kuwataka tena Waajiri kuhakikisha wanatenga bajeti ya moving expenses kwa sababu wanajulikana wale watumishi ambao wanakaribia kustaafu. Sasa ni wajibu wa mwajiri kuangalia wale wanaokaribia kustaafu mwaka unaofuata wa fedha na kuweza kutenga bajeti hiyo. Kwa hiyo, nirudie tena kuwataka Waajiri wote si tu wa local government, si tu wa Iringa Mjini, lakini taasisi zote za umma kuhakikisha wanatenga bajeti kwa ajili ya watumishi wao katika hii moving expenses.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali lake la pili, la madaraja ya 2006. Madaraja haya yalisimama kuanzia Mei, 2016 lakini madaraja haya yalianza tena kutolewa mwezi Novemba, 2017 ambapo Serikali ilipandisha jumla ya watumishi 55,000 Novemba, 2017. Hii ya kutoka 2016 madaraja haya yalikoma kupisha uhakiki uliokuwa ukiendelea, lakini sasa tunaangalia ni namna gani bora ya kuweza kuleta msawazo ili kulindi ile Seniority katika eneo la kazi na Serikali bado inalifanyia kazi suala hili na litakapokuwa tayari tutatolea maelezo zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.