Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 3 2022-02-02

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU Aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha kipengele cha “moving expenses” kilichotolewa ili watumishi walipwe fedha za nauli wakati wakisubiri mafao mengine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, Kanuni J(1) na J(8) ya Kanuni za Kudumu Katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009 pamoja na Waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2008, kipengele cha moving expenses hakijaondolewa. Hivyo, Serikali imekuwa ikigharamia usafiri yaani nauli kwa watumishi wa umma kwa kuzingatia utaratibu ulioelezwa kwa kuzingatia Kanuni tajwa hapo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni J(6)(1) ya Kanuni za Kudumu Katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009 Mtumishi wa Umma hulipwa gharama za usafiri yaani nauli, yeye, mwenza wake na watoto au wategemezi wasiozidi wanne wenye umri chini ya miaka 18 pale anapoajiriwa, anapohama au utumishi wake unapokoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni haki ya kila mtumishi anapostaafu kulipwa gharama za usafiri kurudi mahala atakapoishi baada ya kustaafu, ni wajibu wa kila mwajiri kuhakikisha anatenga fedha za “moving expenses” kwenye bajeti. Hivyo, nitumie nafasi hii kuwakumbusha na kuwataka waajiri kutenga fedha hizi na kutekeleza wajibu wao. Aidha, nichukue fursa hii kuwataka waajiri wote kuandaa orodha ya watumishi wanaokaribia kustaafu na hivyo kurahisisha kubaini gharama halisi zitakazohitajika kuwasafirisha na kuzitenga kweye bajeti kwa ajili hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Kanuni J(8) ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009 pamoja na Waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2008 kuhusu usafirishaji wa mizigo yaani personal effects ya watumishi wa umma, imeeleza namna ya kusafirisha mizigo ya mtumishi wa umma pale anapohama au utumishi wake unapokoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kulipa gharama za kusafirisha watumishi wa umma, familia zao pamoja na mizigo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.