Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K. S. GULAMALI Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Ziba Wilayani Igunga aliyoitoa wakati wa Kampeni za uchaguzi 2020?

Supplementary Question 1

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuweza kutekeleza ahadi za Viongozi wa Kitaifa hasa ilikuwa ni ahadi ya kipindi cha kampeni 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu nipende tu kuuliza kulikuwa na ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuwa amekuja pale Chomachankola. Nilikuwa naomba pia kuweza kupata jibu juu ya Kituo cha Afya cha Chomachamkola ambacho Mheshimiwa Waziri Mkuu alituahidi kutupatia fedha kwa ajili ya kujenga majengo ya wazazi pale. Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Seif Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Seif Gulamali kwa kuwasemea kwa dhati kabisa wananchi wa Jimbo la Manonga na ufuatiliaji wake kuhakikisha Serikali inaendelea kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili nipokee shukrani zake nyingi kwa Serikali na kwa kweli sisi sote Waheshimiwa Wabunge tumeona kazi kubwa sana inayofanywa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya huduma za afya na ndani ya hii miezi sita Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amepeleka zaidi ya bilioni 58 na milioni 250 kujenga Vituo vya Afya 233 kote Nchini. Kwa hivyo, tunapokea shukrani hizi na tuwahakikishie kwamba tutaendelea kushirikiana naye kuhakikisha tunaendelea kuboresha miundombinu hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la Kituo cha Afya ambacho ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba nimuhakikishie kwamba ahadi zote za Viongozi wetu wa Kitaifa zinapewa kipaumbele ikiwemo kituo hiki cha Afya tutaendelea kutafuta fedha na mara zikipatikana tutakwenda kuhakikisha kwamba tunaanza ujenzi wa Kituo cha Afya hicho. Ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. SEIF K. S. GULAMALI Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Ziba Wilayani Igunga aliyoitoa wakati wa Kampeni za uchaguzi 2020?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, matatizo yaliyopo katika Jimbo la Manonga ni sawa kabisa na matatizo yaliyopo kwenye Jimbo la Geita. Kata ya Nkome ina zahanati ambayo kwa mwezi inazalisha watoto wasiopungua 400 na Mheshimiwa Naibu Waziri amefika pale Silinde. Mheshimiwa Waziri juzi tu tumefika ukajionea hali halisi chumba kidogo ukakuta kinamama zaidi ya wanne wanajifungua pale. Sasa nimeshauliza humu mara mbili mara tatu ninapata tu ahadi ambazo hazijatekelezeka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba kupata majibu ya uhakika kwamba ni lini sasa kwa kuwa Mawaziri wote wamefika pale mtanipa fedha ya dharula ili niweze kuwaokoa wale wananchi wa Kata ya Nkome? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Musukuma, kwanza naomba unipe nafasi nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa imani yake kwangu, kwa kunipa majukumu ya kumsaidia katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Rais wetu kwamba, kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu nitatumia maarifa na jitihada zote na kwa ushirikiano wa Waheshimiwa Wabunge naamini mtanipa ushirikiano ili nisiweze kumwangusha Mheshimiwa Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nijibu swali la Mheshimiwa Musukuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli siku si nyingi niliambatana na Mheshimiwa Musukuma kwenda kwenye Jimbo lake la Geita Vijijini. Kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Musukuma kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuwatetea wananchi wake wa Geita Vijijini. Kama nilivyomuahidi Mheshimiwa Musukuma tukiwa Geita Vijijini, muda wowote Serikali tukipata fedha tutaangalia namna ya kuboresha Zahanati ya Nkome ili iweze kuwa Kituo cha Afya ili wananchi wa Kata Nkome pamoja na maeneo ya jirani waweze kupata huduma nzuri kwa mujibu wa Sera ya Kituo cha Afya. Nashukuru.