Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2022-02-02

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K. S. GULAMALI Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Ziba Wilayani Igunga aliyoitoa wakati wa Kampeni za uchaguzi 2020?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISMEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif K. S. Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kujenga Vituo vya kutolea Huduma za Afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuboresha utolewaji wa Huduma ya Afya ya Msingi kwa Wananchi. Ujenzi na Ukarabati wa Vituo unahusisha utekelezaji wa ahadi za viongozi kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika kutekeleza mkakati huu Serikali imepeleka kiasi cha shilingi bilioni 58.25 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vipya vya afya 233 katika Tarafa na Kata za kimkakati ambazo hazikuwa na miundombinu hiyo. Aidha, Serikali imepeleka shilingi milioni 250 katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Ziba ambapo ujenzi umefikia hatua ya umaliziaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mkakati huu Serikali itaendelea kutoa fedha katika Halmashauri kwa ajili ya utekelezaji wa ahadi za viongozi za kujenga au kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.