Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: - Nchi yetu imekuwa na mipango mkakati wa kuzalisha mafuta ya kula kiasi cha kutosheleza soko la ndani. (a) Je, ni kwa nini Serikali isiboreshe mpango ya kuzalisha mafuta ya mawese kimkakati kwa kuhamasisha kilimo cha zao hilo katika Mikoa ya Kagera, Tanga, Pwani, Katavi na Mbeya? (b) Je, ni kwa nini Serikali isitumie mfumo wa kilimo kikubwa cha pamoja (block farming) ambapo Serikali hubeba gharama za awali na hatimaye sehemu ya gharama hukatwa kwenye mauzo ya Mkulima?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada za Serikali kuanzisha block farming kwenye maeneo aliyoyataja kama kwetu Kigoma, maeneo yanayotengwa yanauzwa kwa watu kwamba hekari Tano njoo utoe pesa, lakini mojawapo ya lengo la block farming ni kuwagawia wale wananchi ambao ndio walikuwa wazalishaji wakubwa kwamba Serikali muwabebe halafu mkiwabeba kwa gharama za Serikali ile pesa mliowekeza wananchi watairudisha unapouza.

Kwa nini Serikali sasa msijiandae mkafungua maeneo makubwa mukawatoa Watanzania kwenye nusu heka kwa kaya mkawapeleka heka tano na mkavumilia tunapouza kwa sababu haya mazao ya kimkakati, tutakapouza tukaweza kurudisha hizo pesa kwenye Mfuko wa Serikali? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwijage kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, dhana ya block farming kama alivyoieleza ina njia mbili, aidha Halmashauri ikitenga eneo watu wenye uwezo waweze kununua kuwekeza na kumilikishwa eneo hilo, lakini njia nyingine ni eneo ambalo ardhi inakuwa ni mali ya Halmashauri halafu Wawekezaji wanakuja kuwekeza kwa kupewa long term leasing ambayo wao wanawekeza.

Kwa hiyo, nilitaka nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote kwamba kama Wizara tuko tayari kukutana na Halmashauri yoyote ambayo itakuwa tayari kujadiliana na sisi tutengeneze module ambayo ita attract watu wengi kuweza kuwekeza katika eneo hilo na hilo ni wazo ambalo tunalipokea na tuko tayari kuweza kujadiliana kuweza kufanikisha jambo hilo.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: - Nchi yetu imekuwa na mipango mkakati wa kuzalisha mafuta ya kula kiasi cha kutosheleza soko la ndani. (a) Je, ni kwa nini Serikali isiboreshe mpango ya kuzalisha mafuta ya mawese kimkakati kwa kuhamasisha kilimo cha zao hilo katika Mikoa ya Kagera, Tanga, Pwani, Katavi na Mbeya? (b) Je, ni kwa nini Serikali isitumie mfumo wa kilimo kikubwa cha pamoja (block farming) ambapo Serikali hubeba gharama za awali na hatimaye sehemu ya gharama hukatwa kwenye mauzo ya Mkulima?

Supplementary Question 2

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali wa kupunguza uhaba wa mafuta nchini pamoja na zao la mchikichi lakini Serikali ilitangaza zao la alizeti kuwa ni zao pia litakaloingia kwa ajili ya kwenda kupunguza uhaba wa mafuta ya kula nchini. Katika mkakati huo wa Serikali Waziri Mkuu alitangaza Mikoa mitatu Mkoa wa Dodoma, Singida pamoja na Simiyu kuwa ndiyo Mikoa itakuwa kinara cha uzalishaji wa zao la alizeti.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo kwenye zao hili ni upatikanaji wa mbegu bora pamoja na gharama nafuu, sasa nilitaka kujua Serikali ama Wizara wamejipangaje kwenye suala zima la upatikani wa mbegu bora ambayo pia itakuwa ni bei nafuu itakayoweza kukidhi wakulima wetu kuweza kupata mbegu hiyo?

Mheshimiwa Spika, naomba kupata majibu ya Serikali kuhusiana na zao hili la alizeti. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali tulitangaza zao la halizeti kuwa zao la kimkakati na sisi kama Wizara, ni vizuri Bunge lako Tukufu likafahamu kwamba tumetangaza Mikoa mitatu kuwa ni Mikoa kinara ikiwepo Dodoma, Singida na Simiyu. Hatua tulizochukua kwenye suala la mbegu, Wizara tumeshaandaa jumla ya tani 1,600 za standard seed ya record ambayo tunaiuza kwa shilingi 3,500. Tulichokitaka kutoka kwenye Halmashauri husika ni Halmashauri ilete mahitaji ije tuipatie mbegu, watasaini petition ya makubaliano na Wizara ya Kilimo kuonyesha kwamba hiyo subsidies rate ya shilingi 3,500 fedha yake italipwa namna gani.

Mheshimiwa Spika, tumetoa aina tatu ya namna ya kulipa, cash 50 percent ama kulipa mwisho baada ya mkulima kuvuna, tunawaomba Wakurugenzi wa Halmashauri za Dodoma, Singida na Simiyu tumeshasema tumeongea na Wakuu wa Mikoa na leo tumewaambia Wakuu wa Mikoa tulipokuwa nao kwenye kikao walete. Mheshimiwa Mbunge na wewe karibu umlete Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chemba aje tuweze kukubaliana namna ya kulipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu long term sisi kama nchi tunahitaji high breed seed zaidi ya tani Elfu Tano ili tuweze kuipeleka kwa wakulima. Kwa hiyo, hatua tunayoichukua kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha ni kwamba tutaingia mikataba na wazalishaji binafsi, watu binafsi siyo lazima tuzalishe mbegu Serikali, tutasaini nao makubaliano na wapo watu ambao wameshajitokeza mfano ni mtu anaitwa Ndugu Sumri ambae ana jumla ya hekta 8,000 kule Rukwa tunaingia nae makubaliano tunampa parent seed yeye anatuzalishia sisi serikali, halafu zile mbegu ndiyo tutazi-subsidies ili wakulima waweze kuzipata, ili tuondoke kwenye vicious cycle ya mbegu ni lazima turuhusu sekta binafsi ishirikiane na Serikali na huo ndio mwelekeo wa Wizara, tunaamini baada ya mwaka mmoja ama miwili tatizo la mbegu za alizeti katika nchi litakuwa historia.