Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu hayo yenye matumaini makubwa nataka kujua: Je, ni lini mtaanza ujenzi wa Skimu ya Ilembe ambayo usanifu wa kina uko hatua za mwisho, ikiwa ni pamoja na kumalizia skimu ya Ng’ongo na skimu ya Sakalilo ambazo zimetelekezwa kwa muda mrefu sana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, nataka kujua pamoja na kutambua skimu ya Mititi, Ilembo na Itela, ni lini mtaanza upembuzi yakinifu kwenye skimu hizo muhimu kwa wananchi wa Kata hizo nilizozitaja?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sangu, Mbunge wa Kwela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba skimu hizi kwa muda mrefu zimekuwa idle na hazijafanya kazi yake kwa kiwango ambacho kinatarajiwa. Matatizo mengi ya mifumo yetu ya umwagiliaji imekuwa kwamba skimu nyingi zinajengwa na zinaishia njiani ama zinajengwa mifereji bila kuwa na vyanzo vya uhakika vya maji. Kwa hiyo, hatua ya kwanza ambayo nilitaka nimwahidi kwamba skimu ambazo tumeshazifanyia usanifu, tutaanza kuzitengea fedha kuanzia bajeti ya mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, nimpe commitment; nilimwahidi tulipokuwa wote Rukwa na ninamwahidi tena mbele ya Bunge lako kwamba skimu hii ambayo usanifu wake upo kwenye hatua za mwisho, ni moja kati ya skimu za Mkoa wa Rukwa ambazo tumeshaziweka katika bajeti ya mwaka kesho. Kwa sababu, usanifu tulioufanya ni usanifu kamili kuanzia chanzo cha maji na mifereji mikuu na mifereji ya primary na secondary canals.

Mheshimiwa Spika, la kuhusu kwa ujumla, nataka niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwamba sasa hivi kama Wizara na wiki hii iliyopita Waziri wa Kilimo alituagiza tukae na Tume ya Umwagiliaji. Tumeanza utaratibu mpya kabisa kwenye mifumo ya umwagiliaji kwamba hatujengi skimu nusu nusu, ni heri tujenge skimu moja katika Mkoa kwa ukamilifu, badala ya kupeleka hapa shilingi milioni 50 pale shilingi 100. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, watusubiri tunavyoleta katika bajeti yetu itakayokuja, tutahakikisha Ofisi za Mikoa za Umwagiliaji zinapewa uwezo. Vile vile tutakwenda kufungua Ofisi za Umwagiliaji katika kila Wilaya ili ziweze kusimamia skimu na kuzitambua skimu zote ambazo zipo katika Wilaya zetu. (Makofi)

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 2

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa yanayomkuta Mheshimiwa Sangu huko Kwela yanafanana kabisa na yanayotokea huko Jimboni Buchosa; na kwa kuwa kilimo sasa kimeshathibitika kwamba ni uti wa mgongo na unategemewa na Taifa letu: -

Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kutembelea skimu ya Uchiri iliyopo Buchosa ambayo imetelekezwa kwa muda mrefu, akiwa katika utaratibu wa kuifufua iweze kuwasaidia wananchi wa Buchosa na Taifa kwa ujumla? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Eric Shigongo, Mbunge wa Buchosa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari kwenda kutembelea Jimbo la Buchosa na niko tayari kwenda kutembelea Jimbo la Sengerema kuangalia mabwawa, ambayo fedha zake zilitolewa na hayajafanya kazi vizuri. Kwa hiyo, tutashirikiana Waheshimiwa Wabunge, tutakwenda pamoja. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika skimu ya Mng’aro ambayo Mheshimiwa Waziri mara kadhaa hapa alikuwa anaitolea maelezo; na nimeiuliza lakini bado mpaka sasa fedha zile ambazo mmezitenga shilingi milioni 30 hazijafika kuboresha banio na sasa tunaelekea kuanza kwa msimu wa kilimo: -

Je, ni nini commitment ya Serikali katika jambo hili?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shangazi. Kwanza nimpongeze sana yeye binafsi pamoja na Diwani wake Ndugu Jambia Juma Shehoza kwa kuifuatilia Skimu ya Mnga’ro.

Nataka tu nimwambie kwamba tumeshatangaza tender na tarehe 18 Novemba, 2021 tender hiyo inafunguliwa ili kupatikana Mkandarasi wa kuweza kwenda kuifanya kazi na kurekebisha tatizo la skimu hiyo. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nakushukuru leo kwa kuniona pamoja na ufupi wangu. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya, leo umesimama. (Makofi/Kicheko)

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa ninayoiona katika utengenezaji wa hizi skimu ni ukosefu wa wataalam. Kwa mfano, nimeshtuka sana kujua kwamba Skimu ya Sakalilo mpaka leo eti haijakamilika. Yaani toka kipindi hicho mimi nikiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, wataalam walikuwa wanatoka Mbeya miaka ya 2013 mpaka leo haijakamilika. Kuna tatizo kubwa sana katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, naomba nifahamishwe, Wizara imejipanga vipi kupata wataalam wa kutosha ili kusaidia hizo skimu? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Manyanya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hatua ya kwanza tuliyofanya kama Wizara, kama alivyosema kwamba wataalam walikuwa wanatoka Mbeya. Sasa hivi tumevunja ofisi za kanda na sasa kila Mkoa una Ofisi ya Tume ya Umwagiliaji na tumepeleka manpower, kwa maana ya ma-engineer na kila Mkoa sasa una engineer wa umwagiliaji. Hivi karibuni tumewaruhusu ma-engineer wetu wa Tume ya Umwagiliaji, kuajiri intense ambao ni graduates kutoka University ambao ni ma-engineer wa irrigation waweze kwenda ku-beef up Ofisi za Mikoa.

Mheshimiwa Spika, hatua ya pili ambayo tunajipanga nayo ni kuhakikisha katika kila Wilaya tunakuwa na engineer wa umwagiliaji tukishirikiana na waliopo katika TAMISEMI ili tuweze kuhakikisha kwamba shughuli za umwagiliaji zinasimamiwa. Kwa mwaka ujao wa fedha tutakuwa na ofisi katika kila Halmashauri inayosimamia suala la umwagiliaji ili kuwe kuna efficiency katika kufuatilia miradi ya umwagiliaji na ku-plan ili siku ya mwisho tusifanye kazi hizi nusu nusu.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na miradi mingi ya umwagiliaji ambayo iko chini ya kiwango ambacho kinachotarajiwa na hili ni suala la planning na resource. Nasi kama Wizara tumepeleka mapendekezo yetu Hazina. Tunaamini mwaka ujao wa fedha na Waziri wa Fedha alisema ndani ya Bunge lako wakati anahitimisha kwamba umwagiliaji utakuwa ni sehemu ya kipaumbel. Tunaamini itakuwa hivyo na Bunge lako litatupatia rasilimali.

Mheshimiwa Spika, hatuna tatizo la wataalamu, tuna tatizo la rasilimali fedha ambayo tumeshapeleka kwa wenzetu wa Wizara ya Fedha ili tuweze kutatua hili tatizo. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 5

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali iliahidi kufanya mapitio ya usanifu wa ujenzi wa bwawa la umwagiliaji kwenye eneo la Mto Mkomazi kule Korogwe, lakini mpaka leo ahadi hiyo bado haijatekelezwa: -

Napenda kujua, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa bwawa hilo, kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kwa watu wa Korogwe?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mnzava. Tulifanya ziara akiwepo Mheshimiwa Waziri Mkuu katika Jimbo lake na tuliahidi kupeleka wataalamu.

Nataka tu nimwambie kwamba Wizara ya Kilimo imepatiwa fedha kwa ajili ya Tume ya Umwagiliaji, OC tumeshapokea. Sasa moja ya eneo ambalo wataalam wetu na wasanifu wanakwenda kulifanyia kazi ni eneo hilo. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie tu kwamba kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha usanifu wa bwawa hilo utakuwa umekamilika na tutaliingiza katika plan. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Supplementary Question 6

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Changamoto ya skimu zilizopo Jimbo la Kwela kama ulivyomsikia Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya akiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa; Serikali iliwekeza fedha nyingi kwenye miradi miwili; skimu ya Lwafi pamoja na Katongoro lakini yote haifanyi kazi: -

Mheshimiwa Spika, napenda kupata kauli ya Serikali; Serikali iliwekeza zile fedha zipotee au iliwekeza ili ziwasaidie Watanzania wa Wilaya ya Nkasi? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Aida Khenani Mbunge, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali haijawekeza fedha zile ili zipotee na mapungufu yeye mwenyewe anafahamu, nilikuwa Jimboni kwake na tumeongea kwa kina kuhusu hizi scheme zilizoko katika Jimbo lake, sasa hivi kama Wizara tunafanya hatua za mwisho kupeleka fedha tuliyokuahidi ya Shilingi Milioni 100 ili fedha hizo ziweze kwenda.

Nataka tu nimuahidi kwamba mapungufu yaliyopo katika scheme zilizoko Mkoa wa Rukwa na sehemu nyingi ya nchi ni kwamba nyingi zimejengwa half way, kwa hiyo sasa hivi tunachokifanya ni kuzifanyia tathmini ili tuweze kuzirekebisha ziwe zinachanzo cha maji cha uhakika na mifereji, scheme nyingi zimejengwa mifereji badala ya kuwa na water reserve, kwa hiyo nataka nimuombe yeye pamoja na Waheshimiwa Wabunge, mtupe nafasi ili tuweze ku-rectify haya matatizo yaliyopo. (Makofi)