Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 97 2021-11-12

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha Miradi ya Umwagiliaji ya Ilemba, Ng’ongo, Maleza, Mititi, Itela, Ilembo na Nkwilo katika Jimbo la Kwela?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mpango wa Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji Wilayani (DIDF), kwa mwaka 2008/2009 na mwaka 2009/2010 ilitenga jumla ya shilingi milioni 650,000,000/= kwa ajili ya kuendeleza skimu ya umwagiliaji ya Ng’ongo, yenye ukubwa wa hekta 650 ambazo ujenzi ulianza kutekelezwa mwaka 2012 na kukamilika mwaka 2013. Fedha hizi zilitumika kujenga banio na mfereji mkuu wenye urefu wa mita 1,725 pamoja na miundombinu yake.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kupitia (ASDP II) imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwenye skimu ya umwaguliaji ya Ilembe yenye ukubwa wa hekta 800. Aidha, kazi ya kupima mashamba imekamilika na usanifu wa kina upo hatua za mwisho katika skimu ya umwagiliaji ya Ilembe.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeanza kufanya tathmini ya kina katika miradi yote ya umwagiliaji katika Mikoa ya Rukwa na Katavi. Tathmini hiyo ni pamoja kuangalia kwa kina upungufu kwenye skimu hizo na kutambua maeneo mapya na pia kufanya usanifu wa kina na kutathmini gharama za ujenzi wa miundombinu hiyo ili kuanza kutenga fedha katika bajeti zijazo.