Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Bihawana – Chali hadi Sanza Manyoni kwa kiwango cha lami kwa kuwa barabara hii muhimu huwa haipitiki wakati wa masika? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuinua tuta la barabara katika eneo la Chali ili liweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kutokana na umuhimu wa barabara hii Wabunge wengi waliopita upande wa Bahi na upande wa Manyoni, wamekuwa wanaulizia kuhusu umuhimu wa barabara hii na majibu ya Serikali yamekuwa ndiyo hayo, kwamba, tunatafuta fedha kwa ajili ya usanifu yakinifu na ile nyingine aliyoisema.

Mheshimiwa Spika, sasa, tena niulize hapo: Je, ni lini fedha ya upembuzi yakinifu itapatikana? Maana yake ndiyo hayo hayo miaka yote. Sasa ile ya upembuzi yakinifu na ile nyingine, ni lini fedha itapatikana? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwenye majibu ya sehemu (b) nilikuwa naomba Mheshimiwa Naibu Waziri afanye ziara ili aweze kupata uhakika kabisa na alichokijibu hapa. Mimi mwezi wa Nne nilikesha pale, barabara ilijifunga na kinachojibiwa hapa sicho kilichofanyika. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri baada ya Bunge hili hebu akafanye ziara aweze kuona na mwenyewe awe na picha halisi ya eneo lile.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni lini? Serikali mwaka huu wa fedha imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuanza kazi hii. Suala la kutembelea, hilo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, niko tayari kutembelea hilo eneo kwa sababu ni eneo hili hili tu. Nitakapokuwa nakwenda Kaskazini, basi nitapita barabara hiyo na nitamjulisha ili tuweze kukagua pamoja naye hiyo barabara. Ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Bihawana – Chali hadi Sanza Manyoni kwa kiwango cha lami kwa kuwa barabara hii muhimu huwa haipitiki wakati wa masika? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuinua tuta la barabara katika eneo la Chali ili liweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa leo ni mwaka wangu wa 12 nikiwa Bungeni, Rais wa Awamu ya Nne alituahidi ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama, Nyang’hwale mpaka Busisi na Rais wa Awamu ya Tano naye pia aliahidi hivyo, na leo tuko Awamu ya Sita.

Je, Serikali inatuahidi nini ama inatoa kauli gani kuweka fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya hiyo barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara zote ambazo zimeahidiwa na viongozi wa Kitaifa zinakuwa zimeratibiwa na zinafanyiwa kazi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara ya Kahama kupita Nyang’hwale hadi Busisi ni kati ya barabara ambazo zipo kwenye Mpango na zitaanza kutekelezwa kadri fedha itakavyopatikana. Labda tuangalie kwa bajeti itakayofuata kama fedha itaruhusu na bajeti itaruhusu, basi tutaiweka kwenye Mpango huo ili iweze kufanyiwa upembuzi na usanifu wa kina. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Bihawana – Chali hadi Sanza Manyoni kwa kiwango cha lami kwa kuwa barabara hii muhimu huwa haipitiki wakati wa masika? (b) Je Serikali ina mpango gani wa kuinua tuta la barabara katika eneo la Chali ili liweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Barabara ya Bihawana, Chali, Sanza, Manyoni ambayo imeulizwa na Mheshimiwa Nollo ili iweze kukamilika inahitaji ukamilishaji wa ujenzi wa Daraja la Sanza; na kwa taarifa yako upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishakamilika na fidia ilishatolewa kwa wananchi wa Kijiji cha Sanza: -

Je, nini commitment ya Serikali ya lini ujenzi wa daraja la Sanza utaanza? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, Mbunge wa Manyoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli daraja analosema limeshafanyiwa usanifu na litagharimu pamoja na barabara zake za kuingilia shilingi bilioni 23 na barabara zitakazojengwa ni kilomita kama 14.5. Tunavyoongea, tayari tumetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuanza hiyo kazi. Ahsante. (Makofi)