Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 96 2021-11-12

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Bihawana – Chali hadi Sanza Manyoni kwa kiwango cha lami kwa kuwa barabara hii muhimu huwa haipitiki wakati wa masika?

(b) Je Serikali ina mpango gani wa kuinua tuta la barabara katika eneo la Chali ili liweze kupitika wakati wote?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bihawana – Chali hadi Sanza Manyoni ni barabara ya Mkoa inayojulikana kwa jina la Bihawana - Chidilo – Chipanga – Chali Igongo ambayo ina urefu wa kilomita 69, ambayo inaunganisha Wilaya za Bahi na Manyoni kupitia Sanza. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha za kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 shillingi milioni 759.252 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, sehemu (b) kuhusu kuinua tuta eneo la Chali, Serikali imefanya kazi zifuatazo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2019/ 2020, Serikali imejenga kalavati kubwa na kuinua tuta lenye urefu wa mita 500. Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 Serikali imejenga makalavati makubwa mawili na kuinua tuta lenye urefu wa mita 100. Vilevile, katika mwaka wa fedha huu wa 2021/2022, Serikali imepanga kunyanyua tuta lenye urefu wa mita 500 ambapo mkataba wa kazi hii upo katika hatua za kusainiwa. Ahsante.