Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya kisasa ya kuuzia samaki hasa katika Kata ya Somanga na Kivinje ambazo upatikanaji wa samaki ni mkubwa ili kuboresha maisha ya wavuvi wa Wilaya ya Kilwa kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa kwa muda mrefu wavuvi wadogo wadogo kutoka katika Wilaya ya Kilwa na maeneo mengine ya nchi yetu ya Tanzania wamekuwa hawapati mikopo kutoka kwenye mabenki kwa ajili ya kufanyia shughuli zao mbalimbali za kuboresha shughuli za uvuvi.

Je, Serikali haioni sasa wakati umefika wa kuweza kuwaundia hawa wavuvi wadogo wadogo mfuko maalum ambao wataweza kukopa kwa riba ndogo na hatimae hiyo mikopo iweze kuwanufaisha katika kufanya shughuli zao za uvuvi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Wilaya ya Kilwa kumekuwa na wimbi kubwa la uingiaji wa wafugaji wenye mifugo mingi sana hasa katika Kata za Somanga, Tingi, Kandawale, Njinjo, Mitole, Likawage, Nanjilinji pamoja na Kikole.

Je, Mheshimiwa Waziri ni lini atafika katika Wilaya ya Kilwa ili kuwasaidia wananchi wa Wilaya ya Kilwa kwenda kutatua changamoto mbalimbali zinazotokana na uingiaji wa mifugo mingi katika Wilaya ya Kilwa? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndulane Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Uvuvi kwa ajili ya kuwasaidia wavuvi wadogo wadogo waweze kupata mikopo ya bei nafuu na yenye riba ndogo. Ninaungana na yeye na ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Wabunge wote ambao wanasimamia wavuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa miaka mitano tulionao Wizarani mwaka 2021-2016 wa kuhakikisha tunaupa nguvu uchumi wa blue, jambo hili la kuanzishwa kwa Fisheries Development Fund (Mfuko wa Maendeleo ya Uvuvi) ni miongoni mwa jambo lililopewa kipaumbele. Kwa hivyo, Mheshimiwa Mbunge nikupongeze kwamba umelileta jambo ambalo tayari Serikali imeshaliona na kwa hivyo tunakwenda kulianzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili la kuingia kwa mifugo. Tayari tumekwenda kufanya ziara na nimpe pole sana yeye na wananchi wote, lakini tumekwenda na tumezungumza na makundi mbalimbali, katika Wilaya ya Kilwa nilifika katika Kata ya Nanjilinji kwenda kuzungumza na wananchi pale lakini niko tayari kurejea tena ili kusudi tuweze kufika kule kote alipotaja Mitole, Njinjo, Likawage, Kandawale na hata kule Miguruwe na Zinga Kibaoni, ili kuweza kwenda kuzungumza na wananchi kwa niaba ya maombi haya ya Mheshimiwa Mbunge na hatimaye kuweza kupata suluhu ya tatizo hili kubwa ambalo linawasumbua wananchi wa Kilwa Kaskazini. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya kisasa ya kuuzia samaki hasa katika Kata ya Somanga na Kivinje ambazo upatikanaji wa samaki ni mkubwa ili kuboresha maisha ya wavuvi wa Wilaya ya Kilwa kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na kupongeza kazi nzuri sana inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita, chini Rais Samia ya kufufua uchumi wa Mkoa wa Lindi ikiwemo kufufua mazungumzo ya Mradi wa LNG, lakini pia na utengaji wa shilingi billion 50 kwa ajili ya kujenga Bandari ya Uvuvi Kilwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni lini mchakato huu wa ujenzi wa hii bandari ambao ni ukombozi mkubwa wa ukanda wetu utaanza? Kwa sababu ahadi iliyokuwepo ni kwamba mchakato huu ungeanza mapema pamoja na kumshukuru Mama Samia kwa kazi hii nzuri lakini lini mchakato huu utaanza wa kujenga bandari hii kwa ajili ya uvuvi? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape Moses Nnauye Mbunge wa Mtama Mkoa wa Lindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze sana kwa swali hili zuri na la kimkakati. Ujenzi wa bandari ya Uvuvi umetamkwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020/2025, nasi tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kwake na msukumo wake wa kuhakikisha kwamba mradi huu wa kimkakati wa ujenzi wa bandari unafanikiwa na hatimye kuweza kwenda sambamba na ile zana ya uchumi wa blue. Tayari wataalamu wetu wameshafanya hatua zote za mwanzoni na imekubalika kitaalamu ya kwamba bandari ile itakwenda kujengwa pale Kilwa Masoko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa wataalam wapo katika hatua za mwisho kabisa ya kuweza kuli-demarcate kuliweka sawa lile eneo linalokwenda kuwekwa bandari ile. Na tunashukuru sana kwa kuwa eneo hili ni eneo la kimkakati la kuelekea kule katika bahari kuu. Hivyo kile kilio cha muda mrefu cha Wabunge wengi na Watanzania wengi cha kwamba nchi hainufaiki ipasavyo na bahari yetu sasa kinakwenda kupata muarobaini wake. Kwa kweli tunamshukuru Mheshimiwa Rais hata kwa zile pesa za kununua meli nane ambapo sisi Tanzania bara tutapata meli nne zitakazo kwenda kuvua upande wa bahari kuu. Ninashukuru sana. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya kisasa ya kuuzia samaki hasa katika Kata ya Somanga na Kivinje ambazo upatikanaji wa samaki ni mkubwa ili kuboresha maisha ya wavuvi wa Wilaya ya Kilwa kiuchumi?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, Wilaya ya Hai inawafugaji wengi sana wa ng’ombe wa kisasa, ng’ombe walionenepeshwa lakini pia ng’ombe wale wa kienyeji pia tuna Uwanja wa Ndege wa Kimataifa na tuko tayari kufanya biashara ya Kimataifa ya kuuza nyama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza machinjio ya kisasa katika eneo la KIA ili na sisi tuweze kufungua milango ya kibiashara ya kuuza nyama?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mafuwe Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wafugaji wa Hai ni wafugaji wa ng’ombe wa kisasa wanafuga katika utaratibu ule wa zero grazing, ni katika maeneo yanayofuga vizuri sana na viwanda vidogo vidogo vya maziwa viko pale Hai. Lakini vile vile Hai wanavyo viwanda vya chakula vya mifugo, hongera sana Mheshimiwa Mafuwe na wananchi wote wa Hai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni lini tutajenga machinjio ya kisasa, ninaomba Mheshimiwa Mafuwe wewe na waheshimiwa madiwani wenzako katika Halmashauri ya Hai muanzishe mpango huu, na sisi Wizara ya Mifugo na Uvuvi tutakuwa tayari kushirikiana nanyi katika kuwapa utaalam na mchango mwengine wowote wa kuhakikisha jambo na wazo hili zuri linatimia pale Hai, ahsante sana. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya kisasa ya kuuzia samaki hasa katika Kata ya Somanga na Kivinje ambazo upatikanaji wa samaki ni mkubwa ili kuboresha maisha ya wavuvi wa Wilaya ya Kilwa kiuchumi?

Supplementary Question 4

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, katika jimbo la kawe Kata ya Mbweni kuna wavuvi wengi wadogo wadogo na upatikanaji wa samaki ni mwingi sana lakini wavuvi wele hawana soko la uhakika pale, hawana sehemu maalum ya kuuzia. Ni lini Serikali itajenga soko la uhakika katika Kata ya Mbweni ili kuinua uchumi wa wavuvi wadogo wadogo na kuinua pato la Taifa? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felisha Njau kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika maeneo ambayo yana wavuvi wengi kwenye Jimbo la Kawe wako wavuvi pia. Hapa karibuni nilikwenda kwenye Beach ya Kawe kwa maana ya Kawe Beach, ambako pale lipo Soko la Wavuvi, tayari tumetoa maelekezo kwa wataalam wetu kwenda kuzungumza na viongozi wa eneo lile wakiongozwa na Mheshimiwa Diwani kijana Mheshimiwa Lwakatare, kwa ajili ya kukaa na wavuvi wale na kupanga mpango tuweze kushirikiana na Hamnashauri ya Wilaya ya Kinondoni ambayo ina mapato mazuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi Wizara ya Mifugo na Uvuvi tutashirikiana nayo kuhakikisha kwamba tunatengeneza soko zuri ni mahali pazuri ambako tunaweza kuvua kutengeneza samaki na watu waweze kwenda pale weekends ku-enjoy samaki wa baharini, ni samaki wazuri sana, ahsante sana. (Makofi)