Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 75 2021-11-10

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya kisasa ya kuuzia samaki hasa katika Kata ya Somanga na Kivinje ambazo upatikanaji wa samaki ni mkubwa ili kuboresha maisha ya wavuvi wa Wilaya ya Kilwa kiuchumi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kasmazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa Kata ya Somanga na Kata ya Kivinje ni miongoni mwa maeneo yenye samaki wengi katika Wilaya ya Kilwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 kupitia mradi wa IFAD imetenga fedha kiasi cha shilingi 211,698,940 kwa ajili ya ujenzi wa mitambo ya kuzalisha barafu. Wilaya ya Kilwa ni moja ya maeneo ambayo mitambo ya kuzalisha barafu itajengwa ili kusaidia kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutekeleza mipango ya kuboresha miundombinu ya uvuvi, ikiwemo masoko ya kisasa ya uvuvi katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwa ni pamoja na Kata ya Somanga na Kivinje katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kadri fedha zinavyopatikana. Ahsante. (Makofi)