Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza niishukuru sana Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kazi nzuri ambayo inafanywa kwenye sekta hii muhimu sana ya zao la chai nchini. Nasi wananchi wa Jimbo la Lupembe kwa taarifa tu ni kwamba wananchi sasa wameanza kulipwa mazao yale vizuri, Serikali pia imetupatia fedha kwa ajili ya barabara za kwenye mashamba ya chai, naipongeza sana Serikali na kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Wizara hii ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa, Mpango wa Serikali sasa ni kwenda mbele kuboresha hili zao la chai, Lupembe tulikuwa na mgogoro wa Kiwanda kwa muda mrefu kwa miaka 17 ambao sasa umefikia mwisho. Tumekubaliana kiwanda kirudishwe kwa wabia, kwa maana ya wakulima pamoja na Serikali. Lakini mpaka sasa mchakato wa ukaguzi wa kile kiwanda ili kiweze kukabidhiwa kwa wananchi haujafika mwisho.

Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba ukaguzi huu unafanyika haraka na kiwanda kile kiweze kwenda kwa wananchi ambao ni wakulima wa chai? (Makofi)

Jambo la pili; ndani ya Bunge lako Tukufu pamekuwa na ahadi ya muda mrefu ya Serikali, ya kuanzisha mnada wa zao la chai Dar es Salaam ambapo kwa muda mrefu chai yetu nchini inauzwa Mombasa.

Je, ni lini mnada huu wa chai utaanzishwa nchini Tanzania ili kukuza bei ya chai ya wananchi wa Tanzania? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Enosy, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana na sisi kama Wizara ya Kilimo tunamshukuru kwa dhati kabisa kama Mbunge wa eneo la Lupembe, namna alivyoshiriki katika kuhakikisha kwamba mgogoro uliodumu miaka 17 unafika hatma tunakushukuru sana kwa support uliyoitoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali baada ya huu mgoogro kuwa muda mrefu na mgogoro huu tumeanza kuhangaika nao kwa zaidi ya miaka 17. Hivi sasa tumefikia tamati na tumesaini makubaliano kupitia Solicitor General kati ya pande ambazo zilikuwa zinavutana na hivi sasa ninavyoongea, Kamati kutoka Ofisi ya TR inafanya tathmini ya kuangalia baadhi ya misitu iliyokuwa sehemu ya mgogoro huo na sasa hivi ninavyoongea wako Lupembe wakifanya kazi hiyo na wameripoti siku ya jana katika Mkoa wa Njombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili ni kufanya tathmini ya investment iliyowekwa na mwekezaji ili tuone kwamba, hatutaki siku ya mwisho kudhulumu haki ya mtu. Tunataka hii situation iondoke na tuweze kufanya tathmini kwa hiyo, tunamuomba Mheshimiwa Mbunge atupe muda. Sisi kama Wizara tumeshawasiliana na Wizara ya Fedha na Ofisi ya TR, kuhakikisha kwamba mgogoro huu tunaumaliza mapema. Ili mwakani kiwanda kile kianze kazi chini ya management mpya na yule Mwekezaji tuwe tumemalizana naye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mnada nataka tu nimwambie kwamba dhamira na maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kwamba, mnada huu unatakiwa uanze mwaka huu Disemba.

Mheshimiwa Mwenuekiti, nataka nitoe tu taarifa katika Bunge lako Tukufu leo hii hii tumemaliza kikao cha wadau, kwa sababu wazalishaji wa chai walikuwa wanahofu namna ambavyo tunauweka huu mnada na ile rule book ambayo tunaipitisha. Tumejadiliana na kuweza kukubaliana juu ya mambo yote ambayo walikuwa na hofu nayo. Sasa tunaenda hatua ya pili mnada wa chai unahitaji kuwepo kwa kusajiliwa kwa brokers ambao watafanya hiyo kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na gharama tumekubaliana tutawasajili ma-broker kutoka nchi ya Kenya na kutoka nchi ya Sri Lanka ili mnada wetu uweze kuwa na International Picture na mwisho tutawasajili bure. Leo ndiyo tumekubaliana hivi vitu, nataka nimuombe Mheshimiwa Mbunge na wadau wa chai watupe muda tutahakikisha mnada unatokea, kuna changamoto chai yetu volume ni ndogo, tunaongea na wenzetu wa Burundi ili chai yao nayo ipite katika soko la Dar es Salaam tuko katika hatua nzuri. Tunasaini MOU na Serikali ya Rwanda kati ya Wizara ya Kilimo ya Tanzania na Wizara ya Kilimo ya Rwanda Juu ya namna ambavyo nao chai yao iweze kupita katika mnada wetu. Kwa hiyo, tuko katika hatua nzuri tumeshakuwa na rule book, tumeshamaliza structure zote tumeshaweka platform na sasa tunaanza kusajili madalali watakaoshiriki katika mnada huu na mnada huu utatokea. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa Wilaya ya Hanang’ ni wakulima wakubwa sana wa kilimo cha ngano na wanalima haswa, shayiri na waliingia mkataba na TBL kwa kipindi kirefu juu ya kuwapa mbegu lakini baadae kuwauzia. Kwa hiyo, kuwa na soko la uhakika lakini pia upatikanaji wa mbegu wa uhakika. Mpaka sasa TBL imekaa kimya kwa wakulima na wakulima wamekuwa na taharuki kubwa kwa sababu, msimu umefika na TBL wamekaa kimya.

Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya kuwaondoa hofu wakulima wa shayiri wa Wilaya ya Hanang’? Tunaomba majibu ya Serikali. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halamga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme kauli ya Serikali. TBL hana excuse yoyote kuondoa mfumo wa contract farming wa zao la shayiri. Mwaka jana walitaka ku-withdraw tulikaa nao tukasaini nao makubaliano na walinunua jumla ya tani 8,000 kutoka katika maeneo yenu na leo nimeongea na management ya TBL mimi mwenyewe baada ya kupigiwa simu na Mkuu wa Wilaya watarudi kununua. Kwa sababu, mahitaji yao yote ya incentive package waliyotaka kwa ajili ya kujenga kiwanda hapa Dodoma Serikali imewapatia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie Bunge lako hili Tukufu kuwaambia TBL warudi wakasaini mikataba na wakulima wa Kanda ya Kaskazini kwa ajili ya zao la shayiri kwa sababu, kilio chao Serikali ilisikiliza na tuliwapatia incentive package walizotaka na watapata msamaha wa kodi, tofauti na mzalishaji yeyote wa kinywaji wanachozalisha atakayeagiza shayiri kutoka nje. Hatutoruhusu kuagiza shayiri kutoka nje kabla ya shayiri ya ndani ya nchi kununuliwa. Huu ndiyo msimamo wa Serikali. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Supplementary Question 3

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Changamoto ya wakulima wa Lupembe kwenye eneo la chai ni sawa na changamoto inayowakabili wakulima wa parachichi kwenye Wilaya ya Ngara. Mathalani upatikanaji wa miche bora ya parachichi, masoko pamoja na bei.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatambua wakulima wa parachichi Ngara lakini pia na kuboresha zao la parachichi Ngara? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza yeye ni mdau wa mazao ya horticulture na amekuwa akishirikiana na Wizara katika maeneo mbalimbali. Pili, parachichi ni moja kati ya mazao ambayo kama Wizara ya Kilimo tunayapa priority kubwa kama ni zao ambalo linaweza likabeba sekta nzima ya mbogamboga na matunda. Nataka nimuhakikishie tu kama ana special case zinazohusu Ngara aje Wizarani tukae, tuweze kutatua kama ambavyo tumekuwa tukitatua matatizo ya wakulima wa chai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu miche ya parachichi sasa hivi kama Wizara kupitia TOSCI na TARI, tumeanza mpango wa kutambua wazalishaji wa miche binafsi ambao wanazalisha miche ya parachichi na kuwasajili ili kuweza kulilinda zao hili siku ya mwisho lisiweze kujikuta tunaingia kwenye matatizo kama nchi. Kwa hiyo, nataka nimuombe kama ana jambo specific aje tukae tuweze kujadiliana. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kilimo cha zao la pamba msimu wake ni kipindi hiki na wakulima katika Wilaya ya Kishapu na Mkoa wa Shinyanga kwa ujumla wameshaanza kulima. Lakini Wizara ninaishukuru kwa sababu wamesaidia usambazaji wa mbegu japokuwa siyo kwa wakati. Je, ni aina gani ya mbegu inayotumika sasa hivi katika msimu huu, kwa ajili ya kilimo cha pamba, kwa maana msimu uliopita mbegu tuliyokuwa tunalima haikuwa na tija kwa maana ya uzalishaji wa kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia haikuwa himilivu kwa magonjwa mbalimbali. Kwa hiyo, ninataka nipate majibu Wizara inasema ni aina gani ya mbegu ambayo sasa, ni mbegu rasmi na ndio mbegu inayotumika katika kilimo cha msimu wa mwaka 2021/2022? Pia, ni nini mpango wa kuhakikisha kwamba viuatilifu vinasambazwa kwa wakati? Kwa sababu, kumekuwepo wa ucheleweshwaji wa viuatilifu ili mradi kupambana na aina mbalimbali ya magonjwa katika zao la pamba. Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Butondo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza aina ya mbegu tunayopeleka ni UK08 ambayo tumekuwa nayo kwa kipindi cha kama miaka mitatu, miaka minne sasa hivi. Changamoto iliyojitokeza mwaka jana tumeitatua kwa kuhakikisha kwamba, mbegu tunazozisambaza safari hii zimeshakuwa treated na wakati zinaenda kupandwa tayari mbegu zile zina dawa. Tatizo lililojitokeza mwaka jana ni tatizo ambalo halihusiani sana na mbegu ni tatizo ambalo lilitokana na mambo makubwa mawili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, mbegu zilizoenda zilikuwa hazina dawa ya kupandia ambalo tumelitatua mwaka huu. Jambo la pili ambalo lilijitokeza mwaka jana kule kwenye ukanda wa pamba kuna wale machinga, mbegu ambazo sisi tulizihakikisha zinaenda shambani zikalimwe ziliuzwa na wajanja halafu wakulima waka-replace kwa mbegu yoyote anayoipata barabarani. Kwa hiyo, tumeamua kutengeneza utaratibu upya, tume-control mfumo wa usambazaji na mbegu tumeshaziwekea dawa za awali.

Meshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viuatilifu huu ndiyo mwaka wa kwanza tunaanza na open stock ya milioni 2.5. Kwa hiyo, wakulima watakapopanda tunawapelekea na dawa immediately ili wasiweze kupata matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa maelekezo kuhusu pamba. Tuliamua mwaka huu wakulima wanunue mbegu kwa kujinunulia lakini tumeiona changamoto. Nataka niwaambie wakulima wa pamba na wadau wa pamba, tunafanya jitihada kama Wizara kutafuta fedha ku-finance mbegu hizi ili zao la pamba tuweze kuwagawia wakulima dawa na mbegu bure kama tulivyofanya mwaka jana. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Supplementary Question 5

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wakulima wa Mkoa wa Kagera kwa muda mrefu wamekabiliwa na changamoto ya mnyauko wa migomba na haikupatiwa ufumbuzi. Hivi sasa kumekuja mnyauko na miche ya kahawa kwa hiyo, mkahawa mkubwa unanyauka. Nataka nipate kauli ya Serikali nini mkakati wao wa kuwasaidia wakulima wa Mkoa wa Kagera na hasa Wilaya ya Kyerwa na Karagwe. Kupambana na changamoto ya kukauka kwa mikahawa yao kutokana na hiyo homa ya virusi? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Anatropia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi tu ni kwamba wataalam wa TARI baada ya Wizara kupokea taarifa juu ya athari ya mnyauko wa kahawa, hivi ninavyoongea leo wana zaidi ya siku Saba wako Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kufanya utafiti na kuweza kutafuta solution.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisingependa kutoa jibu fupi ambalo halina uhakika hapa, tusubiri wataalam warudi watatupa majibu lakini tunatafuta solution. (Makofi)