Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 74 2021-11-10

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha zao la chai nchini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la chai linaingizia Taifa fedha za kigeni zaidi ya dola milioni 60 kwa mwaka na kutoa ajira za moja kwa moja kwa zaidi ya watu 50,000 viwandani na mashambani. Zao hili linalimwa katika Wilaya 12 na Mikoa sita ambayo ni Mbeya, Njombe, Iringa, Tanga, Kagera na Mara ambapo wakulima wadogo wa chai wapatao 32,000 hujishugulisha na kilimo cha zao hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inaendelea na jitihada za kuendeleza zao la chai kwa lengo la kuongeza uzalishaji, tija na ubora kwa kutenga fedha za kwa ajili ya utafiti, upatikanaji wa miche bora ya chai, kuimarisha miundombinu, kutoa mafunzo na masoko. Kwa mwaka 2021/ 2022, Serikali imetenga fedha za maendeleo jumla ya shilingi 400,000,000 kwa ajili ya kuzalisha miche 1,000,000; kutoa mafunzo kwa wakulima wadogo na kuendeleza mashamba mama manne yanayosimamiwa na Wakala wa Wakulima Wadogo wa Chai (TSHTDA) ya Korogwe na Lushoto.

Mhasimiwa Mwenyekiti, kupitia Mradi wa AGRICONECT jumla ya Euro milioni tano na laki tano zimetengwa kwa ajili ya kuendeleza zao la chai katika mnyororo wa thamani katika kipindi cha miaka minne inayoishia 2023/2024 katika Wilaya za Rungwe Busokelo, Mufindi na Njombe. Mradi unaotekelezwa na Kampuni za IDH, TRITI na TSHTDA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha shilingi 290,722,500 zimetengwa kwa ajili ya kuzalisha miche 750,000, kutoa mafunzo kwa wakulima hususani kanuni bora za kilimo, kuimarisha Vyama vya Ushirika vipatavyo 34 na kuimarisha huduma za ugani. Miche itakayozalishwa imelenga kutumika kuziba mapengo kwa kuanzisha mashamba mapya. Aidha, ufadhili wa AGRICONEC na kwa kushirikiana na sekta binafsi, Wizara inaratibu uanzishwaji wa mnada wa chai katika kuhakikisha kuwa chai ya wakulima inapata bei nzuri na soko la uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnada huo wa chai nchini unatarajiwa kuanza rasmi mwishoni mwa mwaka huu. Wizara kwa kushirikiana na wadau inakamilisha mkakati wa chai utakaoishia mwaka 2030. Wenye lengo mahususi ya kuongeza tija, uzalishaji wa ubora wa chai, ufanisi katika kutoa huduma za ugani pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kuvutia wawekezaji. Mkakati huu unalenga kuongeza uzalishaji wa chai kutoka tani 33,000 hadi kufikia tani 9,000 chai kavu, ifikapo mwaka 2030 na kuongeza matumizi ya teknolojia katika mnyororo wa thamani na kuimarisha mfumo wa masoko. (Makofi)