Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaruhusu wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Sakale, Kata ya Mbomele, Wilayani Muheza kuanza uchimbaji wa madini ya dhahabu yaliyothibitishwa kupatikana katika kijiji hicho?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIS M. MWINJUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Hata hivyo, ripoti ya NEMC ya Oktoba, 2018 ambayo Mheshimiwa Waziri anaitaja, ilielezea wazi kwamba kinachokatazwa ni uchimbaji mdogo na inashauriwa ufanyike uchimbaji aidha wa kiwango cha kati ama mkubwa, kwa sababu hizo za kimazingira ambazo Mheshimiwa Waziri amezitaja. Sasa je, Serikali haioni kwamba kwa vile wananchi wa Sakale, Kata ya Mbomole, Wilaya ya Muheza, hawana uwezo wa kufanya uchimbaji wa kiwango cha kati ama mkubwa inafaa sasa iwasaidie kupata mwekezaji mwenye vigezo vinavyotajwa na ripoti hiyo ili uchimbaji ule uweze kufanyika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyikiti, la pili; ni ombi kwa Wizara, kwamba tuna maeneo kadhaa mengine katika Wilaya ya Muheza katika Kata ya Pande Darajani katika Kata ya Magila na katika Kata ya Magoroto hasa Kijiji cha Mwembeni ambayo yanaonyesha dalili za kuwa na madini. Je, Serikali inaweza kututumia watalaam wake ili wakafanye tathmini na kuona kama kuna uwezekano wa kuchimba katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda ujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge Hamis Mohamed Mwinjuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kutoa majibu ya Wizara, napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa mwelewa, kwa sababu tulipofanya ziara hii na kukubaliana kwamba uchimbaji mdogo utaleta athari kubwa za mazingira, mara nyingi watu wasingeweza kuamini kwamba mbona kuna mali, lakini tathmini ya kimazingira ilionyesha kwamba uchimbaji mdogo utaleta athari kubwa ambazo yawezekana zisiwe na faida hata kama uchimbaji unafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya kuelewa kwa Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana hata wananchi wote wakaelewa kwamba huenda kama madini haya lazima yachimbwe basi iwe ni kwa uchimbaji wa kati ambao teknolojia yake inakuwa ni ya kuchukua udongo mahali pale na kuchenjulia sehemu nyingine ili kuendelea kulinda vyanzo vya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo, Wizara itatoa ushirikiano wote ambao wananchi wanauhitaji kwa sababu pale tulikwishatoa leseni za uchimbaji mdogo. Kwa hiyo tutawaomba tu wafuate utaratibu, wao watapata muwekezaji halafu watakuja Wizarani, watafanya amalgamation ya uchimbaji mdogo tutazi-upgrade kuwa za uchimbaji wa kati na tutawapa miongozo yote inayostahili ili waweze kufanya uchimbaji ambao bado utazingatia kutoathiri chanzo cha maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili; GST ndiyo taasisi yetu ambayo inakwenda kufanya utafiti wa awali na huwa tunapenda kuhimiza utafiti wa awali kwa sababu hautakuwa ule ambao unaleta na wingi wa mashapo kwa kule chini. Sasa hilo linawezekana, tutawaagiza waje. Mheshimiwa Mbunge hata baada ya hapa anaweza akaja pale ofisini kwetu tukaongea na watu wa GST na wakapanga namna ya kwenda nawe ili awaelekeze katika maeneo ambayo anataka waweze kufanya utafiti ili huo wa awali uweze kuonyesha kama uchimbaji unaweza kuendelea katika vijiji ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaruhusu wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Sakale, Kata ya Mbomele, Wilayani Muheza kuanza uchimbaji wa madini ya dhahabu yaliyothibitishwa kupatikana katika kijiji hicho?

Supplementary Question 2

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Nchi yetu hii imezungukwa sana na wachimbaji wadogo wadogo hasa kwenye maeneo mengi yenye uchimbaji wa madini. Je, ni lini sasa Serikali itarudisha utaratibu uliokuwepo mwanzo wa kutoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo hawa ili kuweza kuwasaidia waweze kupata vifaa na baadaye waweze kufanya uchimbaji wao uwe mzuri zaidi, tuweze kuwapata walipa kodi wazuri zaidi. Ahsante sana.

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kujibu swali la Mheshimiwa Masache, Mbunge wa Chunya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wakati wa nyuma Serikali ilitoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo, lakini nipende kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba utaratibu ule wa ruzuku ama haukueleweka vizuri watu walipokuwa wanachukua na haukuwa na tija yoyote katika kufanikisha malengo yaliyokuwa yamepangwa. Kwa msingi huo Wizara inaendelea kutathimini kuona kama kuna sababu ya kufanya hivyo tena iwe ni wachimbaji wetu wameelewa ili makusudi ya kutoa ruzuku hizo yaweze kufikiwa. Wakati Wizara inafikiria namna ya kufanya hivyo tena tumeona kwamba njia nyingine ambayo inaweza ikawa ni nyepesi ni ya kuyaona mabenki yetu ya ndani, ambapo Mheshimiwa Mbunge ana taarifa kwamba baadhi ya wachimbaji wadogo wadogo katika Jimbo lake la Chunya wamekwishapokea fedha kutoka kwenye mabenki yetu ya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo huo ni utaratibu ambao tunadhani kwamba in the interim kabla ya kufikiria kwamba tunaweza tukawa na wakati mwingine wa ruzuku, basi twende na njia hii ambayo nayo imeanza kuonyesha dalili za kufanikiwa katika kuwasaidia wachimbaji wetu wadogo. Nakushukuru.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaruhusu wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Sakale, Kata ya Mbomele, Wilayani Muheza kuanza uchimbaji wa madini ya dhahabu yaliyothibitishwa kupatikana katika kijiji hicho?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naiuliza Serikali, Mgodi wa Kiwira kwa muda mrefu sana umesimama, je, ni lini Serikali itaamua kuleta wawekezaji au Serikali kuweka nguvu ili kusudi Mgodi huu wa Kiwira uweze kutoa ajira, lakini pia kuipatia pato Serikali yetu ya Tanzania. Ahsante.

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgodi wa Kiwira ni kweli tunatamani kwamba ndani ya Serikali uweze kuanza na wakati wa nyuma tumekuwa tunatamani kwamba taasisi zetu mbili TANESCO pamoja na STAMICO waweze kukaa pamoja na kukubaliana, kwa sababu mgodi ule pamoja na kwamba unatoa tu makaa ya mawe, lakini pia kinatarajia kuwa chanjo kingine cha kutoa nishati na kwa jinsi hiyo inahusisha taasisi zetu mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kusema tu kwamba mwezi Julai, TANESCO pamoja na STAMICO waliwekeana makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja na hivi ninavyoongea Shirika letu la STAMICO lipo katika harakati za ku-mobilize mwekezaji ili mgodi ule uweze kuanza. Nakushukuru sana.