Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 71 2021-11-10

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaruhusu wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Sakale, Kata ya Mbomele, Wilayani Muheza kuanza uchimbaji wa madini ya dhahabu yaliyothibitishwa kupatikana katika kijiji hicho?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, shughuli za uchimbaji mdogo katika eneo la Sakale zilikuwepo kati ya mwaka 2004 na mwaka 2016. Baada ya ziara za viongozi wa Mkoa wa Tanga, Wilaya ya Muheza, Wizara ya Madini pamoja na NEMC na pia Mheshimiwa Mbunge mwenyewe iligundulika kuwa uchimbaji huo unafanyika katika chanzo cha Mto Zigi ambacho ni chanzo kikuu cha maji kwa wakazi wa Muheza na Jiji la Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tathmini ya wataalam wa mazingira iliyofanyika mwaka 2018 Oktoba, ilionyesha kuwa athari za kimazingira ni kubwa endapo uchimbaji utaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muktadha huo na kwa kuhifadhi chanzo cha maji katika bonde la Mto Zigi, uchimbaji mdogo wa dhahabu katika Kijiji cha Sakale, Kata ya Mbomele, Wilayani Muheza hauruhusiwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.