Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITHA E. KABATI aliuliza: - (a) Je Serikali inayo database ya kutambua idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi? (b) Je nini mchango wa Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania katika kipindi cha miaka mitano?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulizie maswali mawili.

Kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake lakini pia niwapongeza Watanzania kwa michango mizuri ambayo wamechangia nchi yetu wanaoishi nje ya nchi. Kwa kuwa Diaspora wakirudi nchini huwa wanachukuliwa kama wageni kwenye nchi yao.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutoa hadhi maalum kwa Diaspora kushiriki ujenzi katika uchumi na uwekezaji kabla hatujaweza kupewa uraia pacha?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, watanzania wanaoishi nje ya nchi wanapopata matatizo kwa mfano kesi, wamekuwa wakipatiwa msaada gani ukiwepo msaada wa kisheria?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge ambaye ni mdau mkubwa sana wa diaspora kwa namna anavyowasemea na kuhakikisha fursa nyingi kwa wana diaspora. Wizara yetu kwa kushirikiana na taasisi za Serikali zote mbili za Tanzania Bara na Zanzibar na kwa kushirikiana na wadau wa sekta binafsi wanaoshughulika na mambo ya Diaspora tayari imeanza kufanya tafiti ili kupitia sera, sheria na taratibu za nchi kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa watanzania wanaoishi nje kupata hadhi maalum.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la pili la msaada wa kisheria wakati wanapopatwa na matatizo kama vile kesi ni kwamba Serikali kupitia balozi zetu zimekuwa zikiwasaidia watanzania wanapopatwa na kesi nje ya nchi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuwatafutia mawakili mabobezi na waaminifu kwa gharama zao; pili, pale kesi inapokuwa katika Mahakama ubalozi umekuwa ukifuatilia kwa karibu sana kesi hizo ili kuona watanzania hawa wanapata haki zao kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi husika.

Mheshimiwa Spika, mwisho pale wanapomaliza vifungo vyao au wanapopata msamaha ubalozi unafanya uratibu wa kuhakikisha kwamba wanarudi nyumbani salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITHA E. KABATI aliuliza: - (a) Je Serikali inayo database ya kutambua idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi? (b) Je nini mchango wa Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania katika kipindi cha miaka mitano?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante kimsingi suala la uraia pacha na Diasporas limefanyiwa mjadala mpana sana kwa muda mrefu sana. Sasa kwa sababu Serikali na niipongeze kwa kufanya jitihada ya kutambua mchango wa Diasporas na tunaamini kwamba wakifungua wakipewa hati maalum ama uraia pacha pamoja na kwamba kuna restriction ya katiba hawaoni sana ifike hatua lifike tamati suala la kujadili masuala la uraia pacha na Diaspora tulifanyie kazi sasa kwa sababu tumeona impact yake ni kubwa zaidi kwa sababu Serikali yenyewe ndiyo imetuambia sasa hiyo ni ndogo tu tukifungua tutapata faida nyingi Zaidi.

Mheshimiwa Spika, sasa Serikali haioni kama imefika hatua tulifanye sasa kwa vitendo suala la kutambua kuwapa hadhi maalum ama kutambua mchango wa Diaspora kiuhalali? Ahsante.

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa watanzania wanaoishi nje ya Nchi na kama nilivyojibu hapo awali ni kwamba tayari saa hivi Serikali inafanya tafiti ya kuangalia vipi tunaweza tukaangalia uwezekano wa watanzania hawa kupewa hadhi maalum. Hivyo namuomba Mheshimiwa Mbunge atupe muda kidogo ili kumaliza tafiti na taratibu hizo ahsante sana.