Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza. Kwanza, nishukuru Serikali yangu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mama Samia Suluhu Hassan jinsi anavyo chapa kazi mwanamama, kweli kinamama tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Waziri na Serikali yake inatambua uchakavu huu wa majengo ya polisi ya Makunduchi pamoja na makazi na wametenga jumla ya shilingi milioni kumi na moja na tisini na tatu mia nne, ambazo fedha hizi zinatakiwa ziende zikafanye ukarabati katika majengo haya na vituo vya polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vituo hivi vimechakaa sana, binafsi ukizingatia Makunduchi ni sehemu ya utalii hususan kila mwaka tunakwenda kule kukoga mwaka na viongozi wetu wakubwa wakubwa wanakwenda kule Makunduchi.

Kwa hiyo, je, Serikali lini itakwenda kuyatengeza majengo haya ili tuondoe kadhia hii ya majengo haya machakavu?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala langu la pili, namuomba Mheshimiwa Naibu Waziri tena nasema tena, Mheshimiwa Naibu Waziri aende mwenye Makunduchi akayaone jinsi yale majengo pamoja na zile nyumba zilivyochakaa. Tuoneeni huruma jamani, tunaona vibaya? Ahsante sana naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NAMBO YA NDANIYA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kujibu masuala mawili mazuri sana ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, Mwantumu Dau Haji nayajibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, moja miongoni mwa azma kubwa ya Serikali hasa kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kupitia Jeshi la Polisi ni kuhakikisha kwamba inaboresha na inatengeneza vituo vyote vya polisi vilivyopo nchini pamoja na nyumba za makaazi za maafisa hawa wa polisi na familia zao. Kwa hiyo, kubwa ni mwambie tu Kituo cha Makunduchi ni moja miongoni mwa kituo ambacho tumeshakipanga na tayari fedha hizi tumo mbioni kuzitafuta na kupitia mwaka wa fedha ujao tutahakikisha kwamba kituo hiki tunakipa kipaumbele ili kijengwe na shughuli za kitalii na mambo mengine yaweze kuendelea vizuri na shughuli za ulinzi na usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo pia, nipo tayari kwenda Makunduchi kwenda kuona hilo eneo ili kuona namna ambavyo tunaweza tukashauri na tukaweza kupata fedha kwa ajili ya kukarabati hicho kituo. Nakushukuru.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mkoa wa Njombe mpaka miaka michache iliyopita ulionekana kama ni mkoa mpya. Katika maeneo yaliyosahaulika kwa Mkoa wa Njombe ni Vituo vya Polisi. Je, Serikali ni lini sasa itaanza kukarabati Kituo cha Polisi cha Mkoa wa Njombe ili kiendane na hadhi ya Mkoa wa Njombe? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo ameliuliza, linalozungumzia suala la ukarabati wa Kituo cha Polisi Njombe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba azma yetu ni kuhakikisha kwamba vituo vyote vinajengwa ipo pale pale. Lakini kikubwa nimwambie tu kwamba tutajitahidi pia katika mwaka wa fedha ujao tuhakikishe kwamba kituo hiki nacho tunakijenga kikawa katika hadhi ile ya kuhakikisha kwamba wananchi wanaweza kupata huduma hizi za ulinzi na usalama. Nakushukuru pia.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 3

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, jengo la Kituo cha Polisi katika Mji Mdogo wa Mlowo ambapo mpaka sasa hivi tayari kimeishawekewa alama ya X kwa sababu kimejengwa kwenye hifadhi ya barabara.

Nilikuwa naomba kufahamu nini mkakati wa Serikali wa kutujengea Kituo kipya cha Polisi pale Mlowo na ikizingatiwa kwamba tayari tunalo eneo ambalo limetengwa pale Forest maalum kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shonza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli moja miongoni mwa changamoto ambazo tuko nazo ni kwamba vituo vingi vipo maeneo ya barabara na wakati Serikali inataka kutanua ama kupanua miundombinu ya barabara inabidi lazima kuna vituo vipitishwe doza kwa ajili ya kuvunjwa ili sasa barabara itengenezwe. Sasa nimwambie tu Mheshimiwa kwamba kwa kuwa eneo lipo, basi tutajitahidi tutenge fedha kwa ajili ya kujenga kituo hicho ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma za ulinzi na usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru pia.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuku kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ningependa kujua kituo cha polisi Mgeta ambacho niliahidiwa kujengwa na niliambiwa nilete tathmini ya ujenzi wa kituo hicho ambacho wananchi wamejenga, tumefikia kwenye boma. Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Naibu mwenye waliniahidi kwamba ikifika mwezi Agosti, 2021 kitakuwa kimeshamalizika kujengwa. Ni lini sasa watakwenda kumaliza hiyo ahadi yao?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Getere nalo nalijibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tulifika wakati tukaona kwamba tunaweza tukapata fedha haraka kwa ajili ya ujenzi wa kituo kile, lakini mambo yaliingiliana kwa sababu tuna nyumba za maaskari, tuna vituo vya polisi, tuna mambo mengi ambayo polisi tunahitaji tuimarishe ili wananchi waweze kupata huduma hizo. Kubwa nimwambie tu kwamba katika mwaka wa fedha ujao tutajitahidi kituo kile tukiangalie, tutakipa kipaumbele ili wananchi waweze kupata huduma za ulinzi na usalama. Nakushukuru.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Wananchi wa Kishapu na wadau wa maendeleo katika Wilaya ya Kishapu wameanzisha jengo kwa maana ya Ofisi ya OCD ya Wilaya ya Kishapu na jumla ya shilingi milioni 60 zimetumika na jengo hilo lipo hatua ya renter. Sasa je, Seikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba ina-suport nguvu za wananchi na wadau ili mradi huduma za kipolisi ziweze kwenda sawasawa katika Wilaya ya Kishapu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniface nalo naomba nilijibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana kwa kuwa ni moja ya miongoni mwa watu ambao wanahamasisha sana wananchi ili kuweza kuanza ile miradi halafu Serikali kwa kupitia wafadhili tuje tuone namna ambavyo tunaweza tukamalizia. Kikubwa nimwambie kwanza, tutajitahidi baada ya Bunge hili tuje tuone hatua hiyo ambayo imefikia hicho kituo ili sasa tuone na sisi tathmini ya kuweza kujenga.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tumwambie kwamba sasa tunakwenda kutafuta fedha, popote zilipo ili tuhakikishe kwamba kituo hiki tunakimaliza na wananchi waweze kupata hizo huduma katika maeneo hayo. Nakushukuru.

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Supplementary Question 6

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, hii habari ya vituo hayo yote tisa lakini kumi kuna Kituo Chukwani kimejengwa kwa nguvu za wananchi na kisha pauliwa tayari. Sasa ni ipi commitment ya Serikali ili kuja kumaliza kituo kile ambacho kinahitaji milioni 30 tu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ali Hassan King, Mbunge na Mtumishi wa wananchi wa Jimbo la Jang’ombe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kiukweli ni kwamba kituo hiki tunakifahamu na binafsi nimeshakwenda kufanya ziara kwenye kituo hiki na hiyo amount ya fedha iliyotajwa tunaifahamu, kikubwa tulimwambia Mheshimiwa Mbunge ambaye alitupeleka katika eneo lile, ilikuwa ni Mheshimiwa Shaha. Mheshimiwa Ahmada Shaha tulikwenda kuona, kikubwa tulichomwambia kwamba sasa tunakwenda kutafuta fedha kwa sababu kama unavyojua siyo jambo la kusema kwamba tunachukua tu kesho tunakwenda kujenga. Ni jambo ambalo linahitaji taratibu za upatikanaji wa fedha kwa hiyo kikubwa nimwambie tu kwamba kituo hicho tunakifahamu na sasa tunakwenda kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.