Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 38 2021-11-04

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali imepanga kuanza kukarabati majengo ya Kituo cha Polisi Makunduchi.?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uchakavu wa Kituo cha Polisi Makunduchi pamoja na nyumba za makazi ya Askari ambayo ni jengo la ghorofa moja linaloishi familia nne na mahanga mawili ya familia kumi na sita. Tathmini kwa ajili ya ukarabati imeshafanyika na jumla ya Shilingi 110,093,400 zinahitajika. Ukarabati huo ni wa kubadilisha paa, dari, mfumo wa maji safi na taka pamoja na kupaka rangi. Jeshi la Polisi linatafuta fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo ikiwa ni pamoja na majengo mengine ya vituo na makazi ya askari yaliyokwisha fanyiwa tathmini. Nakushukuru.