Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiingie makubaliano na Chuo cha Ufundi Lugarawa kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe kwa kupeleka Walimu, vifaa na fedha za ruzuku ili Wanaludewa na Wananjombe wapate mafunzo wakati ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo ukisubiriwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Moja, namwomba Mheshimiwa Waziri aweze kutupa Mpango wa Serikali: Ni kwa muda gani chuo hiki kitakuwa kimekamilika na kuanza kutoa mafunzo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Ludewa kwa umoja wao wamechangia fedha na nguvu zao kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya wanafunzi watakaokuwa na ufaulu mkubwa wa Darasa la Saba.

Je, ni lini Serikali katika kutambua jitihada za wananchi na kuunga mkono juhudi zao? Ni lini Wizara itatuma watalaamu kwa ajili ya kwenda kusajili shule ile ili watoto waweze kuanza kusoma pale?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; naomba sasa kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamonga Mbunge wa Ludewa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Kamonga pamoja na wananchi wa Ludewa na vilevile Watanzania wengine walioko kwenye Mikoa ya Rukwa, Geita pamoja na Simiyu, kwa sababu katika maeneo ambayo vyuo vya mikoa vinaenda kujengwa ni pamoja na maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la muda, tunatarajia ndani ya miezi minane kutoka leo vyuo hivi vinakwenda kukamilika kwa sababu fedha hizi zina muda maalumu wa utekelezaji kuhakikisha kwamba miradi hii inafanyiwa kazi sawa sawa. Kwa hiyo, niwahakikishie tu, Mheshimiwa Rais ametoa fedha hizi kwa kuhakikisha katika kipindi hiki kifupi huduma hizi zinaweza kupatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili, anazungumzia Shule ya Sekondari; nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Ludewa kwamba taratibu za kufuata zipo wakati wa kufanya ukaguzi na kusajili shule hizi. Namshauri Mheshimiwa Mbunge kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri kuweza kuandika barua kupeleka kwenye idara yetu ya Udhibiti Ubora iliyokuwepo katika Wilaya ile ya Ludewa na wataalamu wetu wale wakishapata tu barua na maombi hayo, mara moja wanatakiwa kwenda kwa ajili ya kufanya ukaguzi ili kutengeneza ithibati iwapo viwango vile vimethibitika kuwepo, basi usajili huo utapatikana. Ila kwa vile amelizungumza suala hili hapa Bungeni, tutakwenda kulifanyia kazi kuhakikisha kwamba wiki ijayo wataalamu hao waweze kwenda kwenye eneo hilo la shule ili kuweza kupata usajili ili vijana wetu kama Januari shule hii inaweza kufunguliwa, iweze kufunguliwa na wanafunzi waweze kupata huduma. Ahsante. (Makofi)

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiingie makubaliano na Chuo cha Ufundi Lugarawa kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe kwa kupeleka Walimu, vifaa na fedha za ruzuku ili Wanaludewa na Wananjombe wapate mafunzo wakati ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo ukisubiriwa?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ningependa tu kujua ni lini Serikali sasa itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Kilolo ambayo tayari ina ongezeko la vijana na chuo kinahitajika ili nao waweze kujiendeleza kama ilivyo kwenye maeneo mengine? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba sasa kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivi sasa Serikali inaendelea na ukamilishaji wa vyuo vile vya VETA katika wilaya 29 ambazo sasa zinakwenda kukamilisha, lakini siyo tu kukamilisha na kuhakikisha vile vile vifaa kwa ajili ya mafunzo vinaweza kupatikana. Kwa hiyo katika mwaka huu wa fedha, juhudi za Serikali tunajikita kwenye eneo hilo, kukamilisha vyuo hivi vya wilaya 29, lakini na vile vya mikoa vinne. Kwa hiyo, nimhakikishie, baada ya ukamilishaji wa vyuo hivi, Serikali sasa tunajipanga vizuri kutafuta fedha ili kuweza kufikia wilaya zote kama sera yetu inavyosema kwamba kila wilaya ni lazima iwe na Chuo cha Ufundi cha VETA. Ahsante sana.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiingie makubaliano na Chuo cha Ufundi Lugarawa kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe kwa kupeleka Walimu, vifaa na fedha za ruzuku ili Wanaludewa na Wananjombe wapate mafunzo wakati ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo ukisubiriwa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii. Matatizo ya Ludewa yanafanana sana na matatizo ya Wilaya ya Muleba. Wilaya ya Muleba ni kubwa yenye watoto wengi wanaohitimu darasa la saba, form four na kidato cha sita.

Je, ni lini Serikali itatujengea Chuo cha VETA katika Wilaya ya Muleba? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba sasa kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kikoyo, Mbunge wa Muleba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwa upande wa Kilolo, Serikali inaendelea kutafuta fedha baada ya ukamilishaji wa vyuo hivi 29 katika wilaya 29 ambayo tumeanza kwa awamu ya kwanza kuweza kuzifikia wilaya nyingine ikiwemo na Wilaya ya Muleba. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Kikoyo katika muda mfupi ujao baada ya Serikali kupata fedha tutahakikisha kwamba kila wilaya tunaifikia ikiwemo na wilaya ya Muleba. Ahsante sana.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiingie makubaliano na Chuo cha Ufundi Lugarawa kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe kwa kupeleka Walimu, vifaa na fedha za ruzuku ili Wanaludewa na Wananjombe wapate mafunzo wakati ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo ukisubiriwa?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Jiji la Dar es Salaam lina idadi kubwa ya watu zaidi ya milioni sita na tunategemea Chuo cha VETA kimoja tu maarufu cha Chang’ombe na Wilaya ya Ubungo sasa ipo pembezoni na idadi kubwa ya watu na eneo tunalo: -

Je, ni lini sasa Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Ubungo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kutoa jibu dogo kwa Mheshimiwa Mtemvu Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye maeneo mengine, nitoe rai na wito kwa Mheshimiwa Mtemvu, kwa sababu Ubungo ni Jiji na ni eneo kubwa na mapato yake ni makubwa, kwa hiyo, aone umuhimu nalo wa jambo hili. Basi angalau kwenye mapato ya ndani pale kama wanaweza wakatoa kasma kidogo wakaanza mchakato huu wa ujenzi, pindi pale Serikali itakapopata fedha kwa ajili ya vyuo hivi vya wilaya, basi tutakwenda kuongezea nguvu na kukamilisha chuo hicho.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri naona Wabunge wengi wanauliza vyuo vya VETA huko kwenye maeneo yao, hebu tuambia kwa ujumla mpango wa Serikali kuhusu ujenzi wa vyuo vya VETA. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mpango uliokuwepo hivi sasa kwa mwaka huu wa fedha, bado tunaendelea na ukamilishaji wa vyuo vile 29 na vile vile kununua vifaa. Kwa sababu lengo letu ni kuhakikisha vyuo hivi siyo tunajenga tu majengo, bali vile vile kuhakikisha kwamba tunapeleka pamoja na vifaa ili viweze kufanya kazi na kutoa elimu kwa vijana wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika mwaka ujao wa fedha, jukumu la Serikali ni kuhakikisha kwamba sasa tunaweza kutenga bajeti kwa ajili ya awamu ya pili ya ujenzi wa vyuo vingine vya wilaya. Huo ndiyo mpango uliopo mpaka hivi sasa. Ahsante sana.