Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 34 2021-11-04

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isiingie makubaliano na Chuo cha Ufundi Lugarawa kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe kwa kupeleka Walimu, vifaa na fedha za ruzuku ili Wanaludewa na Wananjombe wapate mafunzo wakati ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo ukisubiriwa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Eilimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa sasa haina utaratibu wa kushirikiana katika kutoa mafunzo kwa pamoja na taasisi binafsi. Hata hivyo, Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na sekta binafsi, zikiwemo taasisi za dini katika utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini. Aidha, Serikali inaendelea kuimarisha taasisi zake za elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwa kujenga vyuo katika ngazi za Wilaya na Mkoa na kuvipatia vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa lengo la kuhakikisha kwamba watanzania wanapata elimu bora ya ufundi karibu na maeneo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mkoa wa Njombe, Serikali inamiliki Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Makete chenye uwezo wa kudahili wanafunzi 160 kwa mwaka. Kwa sasa Serikali inaendelea kupanua Chuo hicho kwa kuongeza madarasa matano yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 100 kwa wakati mmoja, mabweni mawili yenye uwezo wa kulaza wanafunzi 72 kwa kila moja na nyumba mbili za watumishi, kila moja ikiwa na uwezo wa kubeba familia mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia inaendelea na matayarisho kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma cha Mkoa wa Njombe kitakachojengwa katika Wilaya ya Ludewa kupitia fedha za IMF. Aidha, ujenzi wa chuo hicho unatarajiwa kuanza mwezi huu wa Novemba, 2021. Ahsante. (Makofi)