Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasimamia ulipaji fidia kwa Wachimbaji Wadogo wa Kata ya Tumuli?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza niishukuru Serikali ya Mama Samia kupitia Wizara hii, baada ya kilio cha muda mrefu hatimaye wananchi wangu wa Tumuli walilipwa fedha hizo. Pamoja na shukurani hizo naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya wafanyakazi wetu wadogo wa Tumuli, ambao walihamishwa pale katika lile eneo na kwenda kuanzisha maeneo mengine hasa kwa kupelekewa umeme na barabara? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili Serikali ina mpango gani pia kwa kuwasaidia hao wachimbaji wadogo vifaa vya uchimbaji kwa mkopo nafuu haswa hao wa Tumuli, Langida na Ibaga ambao ni wachimbaji wadogo wanaokuza uchumi katika nchi yetu. Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wachimbaji hawa wadogo wa Kata ya Tumuli wanapaswa kuingia katika vikundi, ili watakapokuwa wamekuwa katika vikundi halafu waweze kujisajili na wakishakuwa wamesajiliwa wakatambulika rasmi kama kikundi kilichosajiliwa, basi baada ya hapo taratibu za kuwawekea mazingira bora zinaweza zikaanza ikiwa ni pamoja na kuwapa leseni.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba panapokuwa na uchimbaji wenye tija katika maeneo ya wachimbaji wadogo, tunawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Nishati. Kwamba, kama machimbo hayo yana tija basi waweze pia kupelekewa nishati ya umeme kama ambavyo tumefanya katika machimbo baadhi ya wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Spika, na hili suala la vifaa kwa ajili ya wachimbaji wadogo tumekuwa siku za karibuni tukiwasiliana na mabenki yetu ya ndani, kuona kwamba yanaweza yakaanza kukopesha vifaa kuliko hata fedha zenyewe na katika suala hili pia tumefikia mahali pazuri na hivyo nimpe tu tija Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutaenda tena kuwaona wachimbaji wake kama wameji-organize katika vikundi tutawasajili na baada ya hapo, tutawaunganisha na mabenki yetu ili kwamba waweze kusaidiwa kama ambavyo wengine pia wanasaidiwa hapa nchini. Ninakushukuru sana. (Makofi)