Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 30 2021-11-03

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasimamia ulipaji fidia kwa Wachimbaji Wadogo wa Kata ya Tumuli?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kukusu usimamizi wa Serikali juu ya fidia kwa wachimbaji wadogo wa Kata ya Tumuli, napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa, jitihada za pamoja baina ya Wizara na ufuatiliaji wa karibu sana wa Mheshimiwa Mbunge, mnamo tarehe 9 Agosti, 2021, malipo ya fidia ya shilingi 90,000,000.00 yalilipwa kwa wachimbaji wote 90 wa Kata ya Tumuli na malipo haya yalifanyika chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama ili kupisha uwekezaji wa Kampuni ya PUBO Mining Limited. Ninakushukuru. (Makofi)