Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Supplementary Question 1

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyoneza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nilikuwa naomba kuuliza. Katika mkoa wetu wa Iringa bado kuna maeneo ambayo yanasuasua katika mawasiliano na hasa katika ya Nyazwa, pamoja na kuwa kuna mnara wa Halotel lakini bado kabisa maeneo mengi sana hakuna mawasiliano. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba Mkoa wote wa Iringa kata zote zinapatiwa mawasiliano ya kutosha?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati Mbunge wa Viti Maalum kutoka Iringa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba inafikisha mawasiliano kwa wananchi wote na kuhakikisha kwamba tunaimarisha upatikanaji wa mawasiliano. Lakini naomba kupokea changamoto hii ili tuweze kutuma wataalamu wetu wakafanya tathmini na ili wajiridhishe kchangamoto iko na ukubwa gani ili tuchukue hatua stahiki. Ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Awali ya yote nikupongeze kwa kazi kubwa na nzuri ambayo unaifanya katika Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. ((Makofi)

Mheshimiwa Spika, mawasiliano ni kila kitu katika maisha ya mwanadamu, bila mawsiliano kila kitu kinakuwa siyo sawasawa. Kwa muktadha huo; Jimbo la Mchinga lina tarafa nne ndani ya tarafa mbili angalau klidogo mawasiliano ya simu yanapatikana lakini ndani ya tarafa mbili nyingine, Tarafa ya Milola na Tarafa ya Mipingo hakuna kabisa mtandao. Kukosekana kwa mtandao unasababisha pale kuwa kama kisiwa.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itatuletea mtandao katika Tarafa ya Mpingo na Milola na hasa katika vijiji vya Mipingo, Namakwia, Namkongo, Matakwa na Kiwawa? Ahsante sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete Mbunge wa Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nimpongeze Mheshimiwa Salma Kikwete kwa kuendelea kuwapigania wananchi wake ili wapate huduma ya mawasiliano ili waweze kufanya shughuli zao za kibiashara kama ambavyo Watanzania wangetamani.

Mheshimiwa Spika, lakini kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba tunafiksiha mawasiliano kwa Watanzania wote. Hivyo basi changamoto kama hii inapotokea katika maeneo tofauti tofauti basi kama Serikali ni wajibu wetu kupokea changamoto hii ili tuhakikishe kwamba wataalamu wetu tuwatume katika maeneo specific ili wakapate ukubwa wa tatizo na namna ambavyo tutaenda kulishughulikia kulingana na eneo husika lenyewe. Ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge wa Mchinga amesema, yeye kwake ni tarafa mbili, mimi nina tarafa tano. Kati ya tarafa tano tarafa tatu hazina mawasiliano kabisa. Na utaona hapa sisi wa Lindi tunazungumzia Tarafa, siyo Kijiji, ni tarafa nzaima ambayo ina kata kadhaa na vijiji kadhaa.

Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Serikali, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuja kukomboa Mkoa wa Lindi na suala la mawasiliano kwa sababu pamekuwa na ahadi za miaka nenda, miaka rudi kulimaliza hili jambo?

Hii habari ya kusema tutakuja kutembea ndio majibu yamekuwa haya kila siku. Nataka commitment ya Serikali kuja kutusaidia Mkoa wa Lindi tuondokane na tatizo hili.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape Nnauye Mbunge wa Mtama kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Nape Nnauye kwa sababu amekuwa akitoa taarifa ya changamoto ya mawasiliano ya wananchi wake wa Jimbo la Mtama. Na kwa bahati nzuri nimekaa naye sana na tayari tumeshakubaliana mimi na yeye tutatoka hapa kwenda mpaka Mtama kwenda kujiridisha tukiwa na wataalamu wote kiasi kwamba sasa hili tatizo pindi ambapo tutajua kwamba tatizo lipo wapi ili tuweze sasa kuingiza katika mpango wa utekelezaji wa mwaka ujao. Ahsante sana.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa changamoto iliyopo Jimbo la Nsimbo linashabihiana kabisa na changamoto ya Jiji la Kitalii la Arusha; tunazo kata ambazo zilikuwa zamani Wilaya ya Arumeru kabla hatujawa jiji Kata kama ya Olmoti ambayo ina mitaa ya Nafco na Milongoine, Kata ya Terrat ambayo ina mitaa ya Ulepolosi, Masikilia na Engavunet na Kata ya Olasiti ambayo ina mtaa wa Oloesho bado zina changamoto kubwa ya mawasiliano ya simu.

Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu kwenye kata na mitaa hiyo ambayo nimeitaja?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Mrisho Gambo kwa kazi nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Arusha.

Mheshimiwa Spika, nimeshafika Arusha, na maeneo ambayo ameyataja nayatambua kweli kabisa yana changamoto hiyo. Tayari tumeshaelekeza wataalamu wetu; kwa sababu changamoto ya Arusha si ujenzi wa mnara isipokuwa ni kuongeza nguvu katika minara iliyopo ili iweze kuhudumia wakazi wa Arusha kwa sababu wamekuwa wakiongezeka kwa kasi kubwa hivyo basi minara iliyokuwepo ilikuwa imeshazidiwa nguvu. Tayari wataalamu wetu wameshaanza kufanya kazi na pindi kazi hii itakapokamilika basi changamoto hii itakuwa imeweza kutatuliwa. Ahsante sana.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi pia.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Biharamulo tuna vijiji 75. Kati ya vijiji 75 vijiji 25 havina mawasiliano kabisa, kabisa, na bado tuna shida, ukiachilia mbali vitongoji. Sasa ni nini hatua ambayo Serikali imachukua kwa ajili kuweza kuboresha mawasiliano? Ukizingatia watu hawa nao inabidi washiriki mchango wa maendeleo wa nchi hii lakini wameachwa mbali kwa sababu wako katika maeneo ambayo hayana mawasiliano kabisa. Nataka kusikia kauli ya Serikali kuhusu vijiji 25 vya Biharamulo.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ezra Mbunge wa Biharamulo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Kagera, Wilaya ambayo imebahatika na ambayo itanufaika katika mpango wa utekelezaji mradi wa mipakani basi na Biharamulo inaenda kupata miradi takribani sita.

Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana na kuhakikisha kwamba kipindi kitakapofikia tena cha kuleta bajeti ili tuweze kuhakikisha kwamba maeneo mengi yanapata mawasiliano basi aweze kutuunga mkono kuhakikisha kwamba bajeti hii iweze kwenda kujibu mahitaji ya Watanzania. Ahsante sana. (Makofi)