Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 15 2021-11-02

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika Kata ya Litapunga?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba nimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kufatia mabadiliko aliyoyafanya katika Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na baadaye kuwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kuniteua na kuniapisha kuendelea kuwa Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Taknolojia ya Habari.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Litapunga ina jumla ya vijiji nane ambavyo ni Kaburonge “A”, Kaburonge “B”, Kambuzi “A”, Kambuzi “B”, Kambuzi Halt, Bulembo, Lukama pamoja na Litapunga.

Mheshimiwa Spika, Kata hii imekuwa ikipokea huduma za mawasiliano kutoka kata Jirani za Katumba na Kanoge zenye huduma ya mawasiliano ya Mtandao wa Halotel na Vodacom.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itafanya tathmini ya kiufundi ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika Kata ya Litapunga ili kupata uelewa wa pamoja na ukubwa halisi wa changamoto ili kuelekeza ufumbuzi unaoendana na changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Spika, iwapo tathmini hiyo itabainisha kuwa utatuzi wa changamoto ya upatikanaji wa huduma ya mawasiliano iliyopo unahitaji kuwa na mnara katika kata hiyo, basi Serikali itaingiza kata hii katika zabuni zitakazotangazwa katika siku za karibuni kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.