Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - (a) Je, kwa nini TANESCO imewaondoa watumiaji wadogo wa umeme chini ya unit 75 katika Vijiji vya Itigi, Majengo, Ziginali, Tambukareli, Songambele na Mlowa kuwa Mitaa badala ya Vijiji? (b) Je, ni lini wanavijiji hao watarudishwa katika matumizi ya watumiaji wadogo kwa kuwa hivi ni Vijiji na si Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali, lakini yapo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Singida eneo ambalo linaathirika sana na ukatikaji wa umeme ni eneo la Itigi, lakini na Manyoni wao wanaita feeder ya Manyoni na kila Jumamosi au Jumapili ya wiki lazima umeme ukatike. Sasa je, ni lini zoezi hili litakoma kukatwa katwa umeme katika Halmashauri ya Itigi?

Mheshimiwa Spika lakini pili tunachangamoto ambayo imetokea sasa wakati wenzetu wanaendelea na wakandarasi wa REA nchi nzima katika wilaya ya Manyoni hakuna mkandarasi. je, ni nini tatizo na ni lini mkandarasi wa REA III atapatikana katika Halmashauri za Manyoni na Itigi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Massare kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nianze na swali la pili la Mkandarasi wa REA. Ni kweli kwamba Serikali ilitangaza kazi za kutengeneza umeme wa vijijini na maeneo mengi yakawa yamepata wakandarasi, lakini maeneo Matano yalibaki bila kupata wakandarasi ikiwemo Singida kwa maeneo ya Itigi na Manyoni ni mojawapo.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa taarifa kwenye Bunge lako Tukufu kwamba Ijumaa ya wiki iliyopita, Mkandarasi anayeitwa TungTang amesaini mkataba wa kupeleka umeme katika Wilaya zetu za Itigi na Manyoni na
tumemwambia aripoti kazini Jumatatu ijayo wakati sisi ofisini Serikali ikiwa inaendelea kukamilisha utaratibu wa malipo ya awali.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kusema kwamba, lot ya Singida iko pamoja na lot ya Shinyanga, Tanga na Arusha. Wakandarasi wote hawa tunatarajia waanze kuripoti katika maeneo yao ya kazi kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la kukatikakatika kwa umeme, nianze kwa kusema kwamba tunaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo inaonekana wazi kabisa kwamba kuna mabadiliko makubwa ambayo yamefanyika katika Wizara ya Nishati, lakini katika Shirika letu la TANESCO na tunatarajia kabisa kwamba katika kipindi kifupi kijacho wenzetu ambao wamepewa dhamana sasa TANESCO wataenda kukidhi yale mahitaji ambayo Watanzania wanayatarajia.

Mheshimiwa Spika, siyo hilo tu, bajeti ya TANESCO sasa imewekewa mechanism ya kuhakikisha inaongezeka kwa kuziba ile mianya iliyokuwa ikiachia mapato yavuje ili kuweza kupata nguvu zaidi sasa ya kuimarisha maeneo hayo ya kukatika kwa umeme. Kukatika kwa umeme kunasababishwa na sababu nyingi nyingi, lakini zile ambazo ziko ndani ya uwezo wetu tunahakikisha kwamba tunazifanyia kazi ili tatizo hilo liweze kwisha, siyo kwa Itigi na Manyoni peke yake, lakini kwa nchi nzima. Naomba kuwasilisha.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - (a) Je, kwa nini TANESCO imewaondoa watumiaji wadogo wa umeme chini ya unit 75 katika Vijiji vya Itigi, Majengo, Ziginali, Tambukareli, Songambele na Mlowa kuwa Mitaa badala ya Vijiji? (b) Je, ni lini wanavijiji hao watarudishwa katika matumizi ya watumiaji wadogo kwa kuwa hivi ni Vijiji na si Mitaa?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, pia Halmashauri ya Mji wa Ifakara Jimbo la Kilombero imekuwa ikikosa umeme kila Jumanne na Alhamis; na tunamradi mkubwa sana wa Serikali wa zaidi ya shilingi bilioni 20 wa kituo cha kukuzia umeme. Ujenzi huo wa mradi unasuasua kwa muda mrefu sana: -

Je, Naibu Waziri atakuwa tayari kutembelea pale kutazama changamoto za kusuasua za mradi ule?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako nipo tayari kwenda kuangalia changamoto hizo, lakini niseme kwamba kama anasema ni Jumanne na Alhamis, basi nitafanya mawasiliano na wenzangu tufahamu shida ni nini?

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie Watanzania kwamba hatuna mgao kwa nchi yetu ya Tanzania kwa sasa. Tunao umeme ambao unatosheleza mahitaji tuliyokuwa nayo kwa kile kiasi tunachoweza kupeleka, lakini tutaenda kuangalia tatizo ni nini ili tuweze kulitatua.

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - (a) Je, kwa nini TANESCO imewaondoa watumiaji wadogo wa umeme chini ya unit 75 katika Vijiji vya Itigi, Majengo, Ziginali, Tambukareli, Songambele na Mlowa kuwa Mitaa badala ya Vijiji? (b) Je, ni lini wanavijiji hao watarudishwa katika matumizi ya watumiaji wadogo kwa kuwa hivi ni Vijiji na si Mitaa?

Supplementary Question 3

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Spika ahsante, kwa kuwa ni swali la msingi liliulizia bei ya umeme, nami niulize ni lini TANESCO itatausha bei ya umeme inayouza ZECO?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ali King kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, TANESCO kwa maana ya Shirika la Umeme Tanzania imekuwa na mkataba na Shirika la ZECO kwa maana ya Shirika la Umeme la Zanzibar kwenye kuuziana umeme. Tumekuwa na bei ambazo zinatofautiana; na tumekuwa tuna majadiliano kwa muda mrefu katika eneo hili na jambo hili likapelekwa mpaka kwenye kamati zetu zinazoshughulikia maswali ya na Muungano.

Mheshimiwa Spika, issue kubwa ilikiwa ni habari ya bei. TANESCO walikuwa wanaona wakiuza umeme kwa shilingi 130/= ambayo wenzetu wa ZECO wanaihitaji hawataweza kwa sababu itakuwa ni hasara. ZECO wanasema sisi tukiwauzia kwa shilingi 156/= ambayo tunaona ni gharama za chini za kuzalisha, hatutaweza kufanikiwa kwa sababu ZECO wanasema hiyo kwao ni gharama kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kumekuwa na mazungumzo yanayoendelea na suala hilo limepelekwa katika Kamati ile inayoshughulikia masuala ya Muungano na tunasubiria maelekezo ya Serikali ili kuona namna gani tunaweza kusaidia mashirika haya mawili yaweze kuendelea kushirikiana na kukamilisha upelekaji wa umeme kwa gharama nafuu kwa wenzetu wa Zanzibar. (Makofi)