Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 6 2021-11-02

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

(a) Je, kwa nini TANESCO imewaondoa watumiaji wadogo wa umeme chini ya unit 75 katika Vijiji vya Itigi, Majengo, Ziginali, Tambukareli, Songambele na Mlowa kuwa Mitaa badala ya Vijiji?

(b) Je, ni lini wanavijiji hao watarudishwa katika matumizi ya watumiaji wadogo kwa kuwa hivi ni Vijiji na si Mitaa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Agizo la kurekebisha bei la EWURA Na. 2016-010 la Mwaka 2016, kupitia masharti Namba (h) na (i) inaelekeza TANESCO, kuwaunganisha wateja wapya wa majumbani walio maeneo ya vijijini katika kundi la D1 yaani Domestic 1. Kupitia mfumo wa njia moja ya umeme na wateja walio katika kundi la D1 watahamishiwa kwenda T1 ambayo ni Tariff 1. Endapo manunuzi yao katika kipindi cha miezi mitatu mfululizo yatazidi wastani wa unit 75 kwa mwezi.

Mheshimiwa Spika, wateja wa Itigi walihamishiwa kwenda kundi la T1 kwa kuwa wapo Itigi mjini. Kwa sasa, TANESCO inaendelea kuchambua hali ya ununuzi wa umeme kwa wateja hawa. Kwa lengo la kubaini waliokidhi vigezo vya kuwa kwenye kundi la D1 kwa mujibu wa Agizo la EWURA. Zoezi hili linatarajia kukamilika ifikapo tarehe 30 Novemba, 2021. Baada ya zoezi hili kukamilika wanaostahili kuwa kwenye kundi la Tariff D1 watapelekwa kwenye kundi hili Disemba, 2021.