Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya Wavuvi wa ukanda wa Pwani ili kuchochea uchumi?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga soko kuu la kuuzia samaki kwa Mkoa wetu wa Tanga na ni lini ujenzi utaanza?

Mheshimiwa Spika, swali namba mbili; ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wavuvi wa maeneo ya pembezoni kwa maeneo ya Moa, Chongoleani, Kipumbwi na Mkoaja kuuza samaki wao kwenye soko la pamoja kukwepa wachuuzi kuwachuuza kwa bei ndogo? ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Tanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika majibu ya msingi nimeeleza kwamba kwenye bajeti ya mwaka huu na kupitia ufadhili wa Shirika la IFAD, upo mpango wa Serikali wa kujenga masoko ya samaki. Na soko hili litajengwa katika Wilaya ya Pangani katika Kijiji cha Kipumbwi litakuwa ni soko zuri kubwa na la Kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ameuliza je watauzia wapi wavuvi wa Chongeleani, Mkinga, Kipumbwi na kwingineko. Naomba nimhakikishie kwamba soko hili litakapokuwa tayari, wavuvi wa maeneo yote aliyoyataja watafaidika kwa ajili ya kuuza bidhaa zao, ahsante sana.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya Wavuvi wa ukanda wa Pwani ili kuchochea uchumi?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTER D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, wavuvi wengi wadogowadogo katika ukanda wa Pwani Jimbo la Kawe hasa katika Kata za Msasani, Kawe, Mbweni na Kunduchi wanachangamoto kubwa ya mtaji wa kununua vifaa vya kisasa stahiki ambavyo vinaweza kuwasaidia kupata samaki kulingana na taratibu za kisheria. Ni nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha wavuvi hawa wanapata vifaa hivyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza kutoka kwa Mheshimiwa Njau kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mtaji kwa wavuvi ni moja ya Sera yetu ya Serikali na Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imesisitiza katika kuweka mazingira rafiki ili kusudi wavuvi wetu waweze kupata mikopo.

Mheshimiwa Spika, katika hili, kwa kutumia dirisha lililopo Benki yetu ya Kilimo, iko mikopo kwa ajili ya wavuvi na wadau wanaoshughulika na masuala ya uvuvi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimuombe Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wote wanaotoka katika maeneo ya wavuvi kuhakikisha kwamba wavuvi wanakaa katika vikundi. Na sisi tupo tayari kwenda kuwaunganisha na mabenki na hata kuwapa elimu na mpango mkakati wa namna ya kuandika kuweza ku-access fursa ile ya kupata mikopo, ahsante sana.