Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 112 2021-09-10

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya Wavuvi wa ukanda wa Pwani ili kuchochea uchumi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Mzamili Zodo, Mbunge - Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha mazingira ya wavuvi wa Ukanda wa Pwani, Serikali inafanya yafuatayo: -

(i) Serikali imeweka mazingira rafiki kwa wavuvi kupata mikopo ya masharti nafuu kutoka taasisi mbalimbali za fedha;

(ii) Kupitia ufadhili wa Shirika la IFAD, Serikali inaboresha masoko ya mazao ya uvuvi pamoja na kuweka miundombinu wezeshi ya kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi na;

(iii) Kupitia Taasisi ya Utafiti a Uvuvi (TAFIR), Serikali inatarajia kuweka vifaa vya kuvutia samaki katika Bahari ya Hindi kwa ajili ya kusaidia wavuvi kupata samaki kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali inaendelea na programu ya kuainisha maeneo yenye uvuvi wenye tija kwa kutumia satellite ili kuwataarifu wavuvi maeneo ambayo samaki wanapatikana kwa wingi, ahsante.