Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Mkandarasi wa umeme wa REA ataanza kazi ya kusambaza umeme katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Nishati na ni kweli mkandarasi yupo site anaendelea na kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa vijiji 11 vya awali vilivyopata umeme awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu umeme ule ulipita barabarani bila kupita mitaa yote katika vijiji hivyo kama ville ilivyo Azimio, Chiwana, Mbesa pale Tuwemacho na Ligoma. Ni lini sasa Serikali itaona haja ya kupeleka kuanza mradi wa ujazilizi katika vijiji hivyo ili vitongoji vyote vilivyopo kwenye vijiji hivyo vipate umeme.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba plan na maelekezo ya Serikali ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote 12,268 vinapata umeme ifikapo Desemba mwakani na hilo sisi kwa kutekeleza maelekezo ya Serikali tunaiahidi umma kwamba tutakamilisha maelekezo hayo kwa kadiri ilivyoelekezwa na ilivyoazimiwa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la vitongoji, upelekaji wa umeme kwenye eneo la vitongoji ni zoezi endelevu ambapo wenzetu wa TANESCO wanaendelea kupeleka umeme katika maeneo hayo lakini pia vipo vitongoji vingi ambavyo vitaguswa na Mradi huu wa REA III round two. Lakini specifically upo mradi wa vitongoji ambao ni wa densification yaani umeme jazilizi ambao tunatarajia uanze mwenzi wa 10 mwishoni ambao utahusika pia katika kupeleka umeme kwenye vitongoji alivyovitaja katika Jimbo la Tunduru Kusini. Nashukuru.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Mkandarasi wa umeme wa REA ataanza kazi ya kusambaza umeme katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, changamoto ambayo ipo kwa Mheshimiwa Mpakate kuhusu umeme wa REA pia ipo Makete ambapo mkandarasi aliyemaliza kutekeleza mradi wake yeye anasema amemaliza lakini bado tuna changamoto ya kwamba kuna Vijiji kama Mago, Mbela na Kinyika ambako tuna zaidi ya nyumba 1,000 ambazo wananchi wameshasuka umeme toka 2019 lakini hadi ninavyozungumza muda huu wananchi hao hawajaingiziwa umeme kwa sababu ya kwamba mita na nguzo zimeisha.

Je, ni ipi kauli ya Serikali kwa huyu Mkandarasi wa REA ambaye hajakamilisha kazi yake ipasavyo ndani ya Jimbo la Makete na wananchi wangu wanaendelea kuteseka? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunapompatia mkandarasi kazi, tunampa wigo wa kufanya kazi ambayo tunaita ni wateja wa awali. Na kwa wakandarasi wa REA III Round One wako wakandarasi kama wanne ambao walikuwa hawajakamilisha kazi zao ambao tumewaelekeza ifikapo mwishoni mwa mwezi wa 10 wawe wamekamilisha kazi zote. Hivyo, tunatarajia kuanzia mwezi wa 11 hakutakuwa kuna mkandarasi ambaye alikuwa anafanya kazi tofauti na REA III Round Two ambaye atakuwa bado yupo kazini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baaada ya hapa nitafuatilia na kujua hivyo vijiji vilivyobaki ni vingapi na avikamilishe kwa sababu kwenye REA III Round Two hatutaacha kijiji hata kimoja ambacho hakitapata umeme ifikapo Desemba mwakani. (Makofi)