Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 111 2021-09-10

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, ni lini Mkandarasi wa umeme wa REA ataanza kazi ya kusambaza umeme katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza umeme nchini kuanzia Mwezi Mei, 2021 ambapo Kampuni ya M/S Guangdong Jianneng Electric Power Engineering Co. LTD imepewa kazi hiyo katika Wilaya ya Tunduru ikiwa ni pamoja na Jimbo la Tunduru Kusini.

Mheshimiwa Spika, kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilomita 639 za njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33, njia za umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 80, ufungaji wa transfoma 80 na uunganishaji wa wateja wa awali wapatao 1,760. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 36.67.

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi kwa sasa anakamilisha usanifu wa kina na uletaji wa vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya umeme. Mradi unatarajiwa kukamilika Mwezi Desemba, 2022 na kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote 80 vilivyokuwa vimebaki bila umeme katika Wilaya ya Tunduru.