Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Utalii Nyanda za Juu Kusini katika eneo la Kihesa – Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nilikuwa nina maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza, Serikali ina mpango gani pia kuendelea kutoa vibali kwa ajili ya wale wawindaji waliokuwa wakifanya uwindaji katika mbuga zetu za nyanda za juu kusini?

Mheshimiwa Spika, pia Serikali ina mkakati gani wa kushirikiana na Wizara ya Fedha ili kuboresha huduma za upatikanaji wa fedha za kigeni ili kuwarahisishia watalii nchini hasa kwa kuruhusu maduka ya kubadilisha fedha za kigeni?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameulizia kuhusu vibali vya uwindaji. Vibali vya uwindaji vimeendelea kutolewa na Wizara kama kawaida na wafanyabiashara kwa maana ya wawekezaji wote ambao wanatamani kuja kuwekeza kwenye eneo hili la uwindaji, tumekuwa tukitoa vibali kupitia mbinu mbalimbali ikiwemo ya kupitia manunuzi ambayo tunatangaza kwa njia ya kieletroniki. Kwa hiyo, ninawaalika tu wawekezaji ambao wanataka kuwekeza katika sekta hii ya uwindaji waje na kila baada ya muda tunapokuwa tumefanya matangazo haya kuna ambao wanapata lakini wanaochelewa, tunaendelea kutangaza kila baada ya muda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye upande wa kubadilisha fedha kwenye maduka haya ya fedha za kigeni, mpaka sasa Serikali imeendelea kushirikiana na hao wafanyabiashara ikiwemo kuandaa mazingira mazuri kwa ajili ya kuendelea na biashara hii ya kubadilisha fedha. Tunawaomba tu wale wafanyabiashara wote ambao wanafanya biashara hizi waendelee kufuata taratibu wa Serikali kama ambavyo imeendelea kuelekezwa na Wizara ya Fedha. Nasi Sekta ya Maliasili na Utalii tutaendelea kuungana nao pamoja ili kuhakikisha kwamba biashara hii inaendelea kufanyika ili tuweze kukuza utalii katika nchi yetu. Ahsante.