Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 108 2021-09-10

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Utalii Nyanda za Juu Kusini katika eneo la Kihesa – Kilolo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iko kwenye hatua za awali za ujenzi wa jengo la kituo cha utalii katika eneo la Kihesa -Kilolo Mkoani Iringa, kupitia mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania - REGROW. Hadi kufikia mwezi Julai, 2021, Wizara imeajiri Mshauri Mwelekezi ambaye anaendelea na kazi ya kutengeneza Mpango wa Biashara na upembuzi yakinifu pamoja na usanifu wa awali wa kituo hicho. Aidha, Mshauri Mwelekezi ameshawasilisha taarifa ya awali.

Mheshimiwa Spika, lengo la kituo hicho ni kutoa huduma za utalii ikiwa ni pamoja na vibali vya kuendesha utalii, kutoa taarifa zinazohusiana na maeneo ya uwekezaji wa utalii na pia kuweka jukwaa kwa sekta binafsi kukaa pamoja na kujadiliana fursa na changamoto mbalimbali katika Sekta ya Utalii ikiwa ni pamoja na kupeana uzoefu kwenye kutoa huduma kwa watalii katika sekta hiyo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.