Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule za Sekondari za Lesoit, Dosidosi, Ndedo na Dongo kuwa Kidato cha Tano na Sita kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Kidato cha Tano na Sita Kiteto?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mengine mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa sasa halmashauri na wananchi kwa kweli wamewekeza nguvu kuboresha miundombinu ya mabweni, vyoo, madarasa, mabwalo katika shule hizi za Dosidosi, Dongo, Ndedo na Lesoit, nini commitment ya Serikali sasa kama kuwaongezea nguvu katika jitihada hizi za kuboresha miundombinu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kwenda na mimi Kiteto kwa siku ambazo sio nyingi sana tutembelee shule hizi za Dongo, Lesoitd, Ndedo, Dosidosi na Sunya ili kuona mazingira yalivyo ili tuweze kushauriana? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Edward Olelekaita Mbunge wa Jimbo la Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza anataka tu commitment ya Serikali kutokana na jitihada kubwa iliyofanywa na wananchi wake katika Jimbo la Kiteto. Nikiri tu kwamba moja ya mpango wa Serikali katika Mwaka huu wa Fedha ni kuongeza upanuzi wa shule 100. Katika hizo shule 100 lengo letu ni ili ziweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita. Kwa hiyo, niseme tu kwamba, miongoni mwa shule tutakazozingatia ni pamoja na maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha katika ule mpango wetu wa shule 100. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili la kwenda Kiteto, nitakwenda. Nitaongozana na Mheshimiwa Mbunge ili tukajionee hayo maeneo husika. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule za Sekondari za Lesoit, Dosidosi, Ndedo na Dongo kuwa Kidato cha Tano na Sita kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Kidato cha Tano na Sita Kiteto?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Shule ya Sekondari Ngh’oboko Halmashauri ilishajenga majengo ya kidato cha tano na sita, madarasa manne yakiwa na ofisi tatu na vyoo 16 vya ndani. Je, Serikali iko tayari kujenga bweni na kukamilisha bwalo ambalo liko usawa wa Hanam likiwa na store ili shule hii iwe na kidato cha tano na sita? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Mbunge hili ombi lake ameshalileta ofisini kwetu na nimeshalikabidhi kwa wataalam waweze kuangalia kwamba wanaweza kusaidia nini. Maombi aliyoyaainisha hapo ni bweni na bwalo, kwa hiyo, nilishalikubali tangu jana alipokuwa ameniletea yale maombi. Kwa hiyo, nimwambie tu kwamba aondoe wasiwasi, Serikali chini ya Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu itafanya hii kazi na tutaifungua hiyo shule ili wanafunzi waanze kusoma.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule za Sekondari za Lesoit, Dosidosi, Ndedo na Dongo kuwa Kidato cha Tano na Sita kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Kidato cha Tano na Sita Kiteto?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pale katika Jimbo la Kinondoni tuna shule za sekondari tisa zenye wanafunzi zaidi ya 11,000 na pass rate pale pamoja na wale wanaokwenda kidato cha tano na sita ni zaidi ya asilimia 80. Hata hivyo, hawa ni watu wa hali ya chini sana, wanapelekwa shule za mbali. Kwa kuwa hatuna high school, naiomba Serikali ikubaliane na mimi kwamba itujengee hata day school ya high school ambayo itaweza kuwasaidia wananchi wa vipato vya kawaida kabisa katika jimbo lile badala ya kuwapeleka mbali wanafunzi wetu. Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba moja ya maelekezo moja ya maelekezo aliyotoa Waziri wa Nchi katika Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam ikiwemo Kinondoni ambazo zina mapato mengi na haya maelekezo tumewaagiza Wakurugenzi kuhakikisha wanatenga fedha kupitia fedha zao za ndani kujenga shule za sekondari ikiwemo kumalizia madarasa katika maeneo ambayo hakuna.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili ambalo wameliomba hapa namwagiza Mkurugenzi wa Kinondoni kuhakikisha hili linatekelezeka nami nitakwenda kufuatilia kuhakikisha hii ahadi ambayo nimeiahidi hapa Bungeni inafanya kazi, Kinondoni wana huo uwezo wa kutekeleza kwa kutumia mapato yao ya ndani. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule za Sekondari za Lesoit, Dosidosi, Ndedo na Dongo kuwa Kidato cha Tano na Sita kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Kidato cha Tano na Sita Kiteto?

Supplementary Question 4

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kuna changamoto kubwa sana katika maeneo ya wafugaji; na kwa sababu wana utamaduni wa kuhama; na changamoto hii iko katika baadhi ya Kata katika Wilaya ya Karatu na Mbulu Vijijini katika eneo linaitwa Yaeda Chini; je, Serikali sasa iko tayari kutazama maeneo haya na kuhakikisha wanajenga mabweni kuanzia Shule za Awali, Msingi na hadi Sekondari ili kuhakikisha kwamba jamii hii ya kifugaji na wenyewe watoto wao wanapata haki ya kupata elimu kama ambavyo walivyo katika maeneo mengine nchini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anaomba kwamba tuendelee kuyazingatia maeneo ya wafugaji na ameainisha hapa eneo la Yaeda Chini na anataka commitment ya Serikali ikiwemo kujenga shule kuanzia awali, msingi na sekondari ili tuweze kuwasaidia maeneo hayo. Nimhakikishie tu kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa ikizingatia kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi, katika eneo ambalo anatokea Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kwamba Serikali ilijenga kule shule. Kwa hiyo, hata maeneo yote ya wafugaji tutaendelea kuyazingatia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutaendelea kuyaweka kwenye mpango kwa kadri fedha inapopatikana na kuhakikisha kwamba tunahudumia wananchi wote ili wapate huduma ya msingi ya elimu ikiwemo hayo maeneo ambayo ameainisha. Ahsante sana.