Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 106 2021-09-10

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule za Sekondari za Lesoit, Dosidosi, Ndedo na Dongo kuwa Kidato cha Tano na Sita kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Kidato cha Tano na Sita Kiteto?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edward Olelekaita Kisau, Mbunge wa Jimbo la Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali inatambua uhitaji mkubwa wa shule za kidato cha tano na sita katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto. Shule tatu ni za bweni na moja ni ya kutwa ambazo zilianzishwa makusudi kwa ajili ya kuwasaidia ndugu zetu wafugaji wanaohamahama ili wasome bila kukatisha masomo. Shule hizo zinashindwa kupandishwa hadhi kutokana na upungufu wa miundombinu ya mabweni, mabwalo na madarasa ya kutosha kwa ajili ya kidato cha kwanza hadi cha nne na kidato cha tano na sita.

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kumwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kiteto akishirikiana na wananachi wajenge mabweni, madarasa na mabwalo kwenye shule hizo ili yatosheleze mahitaji ya wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne na kuongeza mengine ambayo yanaweza kutumika kwa ajili ya kidato cha tano na sita ili tuweze kuzipandisha hadhi shule hizo.