Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima vya maji katika Kata ya Mwamanyili Kijiji cha Milambi Wilayani Busega ili kuwapunguzia adha ya maji akina mama wa Kijiji hicho?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nina penda kushukuru sana kwa majibu mazuri ya Waziri. Lakini nina maswali mawili tu ya nyongeza. Katika Mkoa wa Simiyu kuna Wilaya tano lakini Wilaya ya Meatu ndio ina ukame sana kuliko Wilaya zote hizo tano. Nilipenda kujua ni lini sasa Serikali itachimba visima virefu vya maji na kusambaza katika vijiji hivyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Naibu Waziri yuko tayari kuambatana pamoja nami twende naye katika Wilaya ya Meatu aone wakina mama wanavyopata adha ya maji katika Wilaya ya Meatu? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Minza Mjika kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nipende kupokea pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge. Lakini vile vile nipende kumpongeza na yeye, kwa kazi nzuri anayoifanya kwa ushirikiano mkubwa ndani ya Wizara ya Maji. Amekuwa mfuatiliaji mzuri sana akisaidiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo kaka yangu Simon wanafanya kazi nzuri kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali katika mwaka huu wa fedha 2021/2022 ni kuchimba visima virefu katika Wilaya ya Meatu. Tunatambua namna gani wakinamama wanapata shida ya maji katika Mji ule. Hivyo, tumshukuru Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, ameliona hili na ameshatupatia fedha tutaenda sasa kifua mbele kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuambatana kwangu ni kawaida. Hivyo, niseme Mheshimiwa Minza usiwe na wasiwasi baada ya Bunge hili, baada ya kumaliza ratiba ya Mikoa niliyoipanga nitakuja kwako Simiyu hususani Meatu. Lengo ni kuona hali halisi na kuongeza chachu na ufanisi wa miradi yetu ya maji. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima vya maji katika Kata ya Mwamanyili Kijiji cha Milambi Wilayani Busega ili kuwapunguzia adha ya maji akina mama wa Kijiji hicho?

Supplementary Question 2

MHE. JUMANNE A. SAGINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri kuhusu maji Busega. Lakini tatizo la maji Busega linakaribia kufanana na tatizo la maji Butiama. Huu ni mwezi wa tano kwenye Kijiji cha Butiama cha Baba wa Taifa hawajapata maji na wataalam wanasema ni tatizo la mashine. Sasa Naibu Waziri atuambie lini wananchi wa Butiama wataweza kupata maji kutoka Ziwa Victoria? Na ambapo tayari kuna bomba lililochakaa lakini tatizo ni mtambo unashindwa kusukuma. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sagini, Mbunge wa Butiama kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara tunatambua eneo lile miradi ni mchakavu lakini tayari tumeshaelekeza wataalamu wetu kuweza kuipitia na ukarabati kufanyika, pamoja na mradi wa muda mrefu mradi wa Ziwa Victoria nao upo katika mipango mkakati ya Wizara.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima vya maji katika Kata ya Mwamanyili Kijiji cha Milambi Wilayani Busega ili kuwapunguzia adha ya maji akina mama wa Kijiji hicho?

Supplementary Question 3

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, Jimbo la Tabora Kaskazini vijiji 58 vitapata maji ya Ziwa Victoria. Swali, Je, Serikali ina mpango gani kuchimba visima virefu katika maeneo ambayo bomba la Ziwa Victoria halipiti?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maige Mbunge wa Tabora kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu fika mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria umeweza kufika katika Mkoa wa Tabora. Lakini kwa maeneo ambayo mradi huu hauwezi kufika kwa sababu, bomba kuu linapopita ni kilomita 12 kulia na kushoto wanaweza kunufaika moja kwa moja.

Maeneo ambayo yako ndani zaidi mpango wa Serikali ni kuchimba hivi visima virefu na tayari Serikali imeviandaa visima zaidi ya 500 kwa ajili ya nchi nzima. Hivyo niweze kumtoa hofu Mheshimiwa Maige na yeye ataweza kuingia katika mgao wa visima hivi. Lengo ni kuona kwamba wananchi wenye imani kubwa kwa Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan wanaweza kuhudumiwa na kutuliwa ndoo kichwani. (Makofi)