Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 102 2021-09-09

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itachimba visima vya maji katika Kata ya Mwamanyili Kijiji cha Milambi Wilayani Busega ili kuwapunguzia adha ya maji akina mama wa Kijiji hicho?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama. Serikali itafanya upanuzi wa mradi wa maji wa Mwamanyili ambao chanzo chake ni Ziwa Victoria kwenda katika Vijiji vya Mwamanyili, Mwanangi, Milambi na maeneo ya Nassa Ginery. Upanuzi huo utahusisha ukarabati wa chanzo cha maji, ulazaji wa bomba la urefu wa kilometa 13.6 na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 15. Kukamilika kwa utekelezaji wa mpango huo kutaboresha huduma ya maji hadi kufikia asilimia 54. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mpango wa muda mrefu, Serikali imepanga kutekeleza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Miji ya Busega, Bariadi na Itilima Mkoani Simiyu. Mradi huo utanufaisha zaidi ya vijiji 200 vya Miji hiyo.