Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya ziada ya kudhibiti tatizo la utapeli na wizi wa kimtandao kupitia simu za mkononi?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Wizi wa kimtandao unaongezeka kila kukicha; kwa kuwa TCRA kwa maana ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania wana uwezo wa kujua namba fulani inayofanya wizi ipo mahali fulani: Je, kwa nini Serikali sasa haioni kwamba uwepo utaratibu maalumu wa Jeshi la Polisi pamoja na TCRA kuzuia watu kabla hawajaibiwa kwa sababu wana uwezo wa ku-trace hiyo namba? Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, pale namba inapotumika ambapo namba ile siyo ya kawaida kwa mfano hizi namba zinazoanzia 15000 na kuendelea ndiyo namba ambazo ni za mitandao yenyewe, unakuta zinatuma ujumbe kwa mfano umeshinda labda shilingi milioni 600, umeshinda shilingi milioni sita, umeshinda kiasi kadhaa; anatuma mtu anaendelea kukatwa fedha zake. Sasa nauliza je, pale mwananchi ambapo anakuwa hana kosa na kosa ni la hawa wenye mitandao wenyewe kwa mfano TiGO au Vodacom, kuna mkakati gani wa Serikali ili wananchi ambao hawakufanya makosa yoyote waweze kubanwa hizi kampuni za simu kulipa fedha zao? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nimpongeze Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kwa kazi kubwa anayoifanya kwa maslahi ya wananchi wa Jimbo lake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, naomba niwashukuru na kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa kazi kubwa ambayo wamekuwa wakiifanya kwa kushiriki katika michakato mbalimbali ya kuishauri Serikali ili tuweze kuboresha huduma kwa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo ambalo Mheshimiwa Mwakasaka ameliongelea ni kwamba Serikali inamkakati gani wa kujaribu kuzuia wizi kabla hata haujatokea? Sheria ya makosa ya Kimatandao ya Mwaka 2015 ambayo ilianzishwa mahususi kwanza kutambua makosa yenyewe ya kimtandao ni yapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kikubwa ni kwamba kupitia Kamati ambayo imeshaundwa, kwa nafasi hiyo, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuisimamia vizuri Kamati hiyo, kazi yake kubwa ni kwenda kutoa elimu kwa Umma. Inapotoa elimu kwa Umma ni pale ambapo sasa Mtanzania anajua kabisa kwamba ni kosa lipi ambalo linahusika na sheria hii na kulihalalisha kwamba nikilifanya basi hatua za kisheria zitachukuliwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ni kujenga uwezo kama ambavyo nimesema kwamba kuna kitengo maalum cha makosa ya kimtandao, ambayo ni Cybercrime Unit ambayo inashughulika na makosa haya. Lakini kuwajengea uwezo na kuleta vitendea kazi ambavyo…

NAIBU SPIKA: Elekea kwenye jibu la pili hilo ameshaelewa Mheshimiwa Mwakasaka. Jibu swali lake la pili. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali la pili anaongelea kuhusu message ambazo wanakuwa wanatumiwa. Nalo hili linaangukia katika makosa yale yale ya kimtandao tunasema unsolicited messages. Hili tayari tumeshakaa na watoa huduma tumeshaanza kuweka mkakati wa kuhakikisha kwamba, tunawasaidia na kuelewa kwamba namna gani message hizi hazitakiwi kutumwa kwa watanzania ambao hawajaziomba. Matokeo yake wanakuwa na makosa ambayo hawajahusika moja kwa moja. Ahsante. (Makofi)