Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Sita Mungaa ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kipindi cha Kampeni mwaka 2020 alipopita Jimbo la Singida Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Mungaa ina shule zaidi ya nane za O-level na kwa sababu shule hii ya Mungaa ni kongwe ndiyo maana niliomba shule hii iweze kujengwa ili kuwapatia fursa wanafunzi wanaokosa nafasi ya kwenda kidato cha tano na sita kama ambavyo imekuwa ni tatizo kwenye maeneo mengine.

Kwa hiyo, naiomba Serikali katika tathmini hiyo iweze kuchukua umuhimu wa pekee kuhakikisha shule hiyo inajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika vikwazo ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza ni pamoja na vikwazo vya watoto wa kike katika shule zetu za sekondari zikiwemo shule za kata. Ni nini mkakati wa Serikali kujenga hosteli za kuweza ku-accommodate wanafunzi wote wa kike katika shule zetu ambazo ziko katika Jimbo la Singida Mashariki? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza alikuwa ameelezea tu kwamba Tarafa ya Mungaa ina shule nane za O-level na hivyo alikuwa anasisitiza tu kwamba tuiweke kwenye tathmini. Katika jibu la msingi tumekubali kwamba kwenye tathmini ya zile shule 100 ambazo tunakwenda kuzifanyia upanuzi nchi nzima kwa ajili ya kupokea watoto wa kidato cha tano miongoni mwa shule tutakayoifanyia tathmini ni Shule ya Mungaa. Kwa hiyo, hilo tumelikubali litafanyika katika mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili kuhusu vikwazo kwa watoto wa shule ambao wanatembea umbali mrefu kuelekea shuleni, moja ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais mama yetu Samia Suluhu Hassan ni pamoja na kujenga hosteli. Ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha tumetenga fedha nyingi tu kuhakikisha kwamba tunajenga hosteli katika maeneo mbalimbali na ninyi mmepitisha bajeti hiyo. Kwa hiyo, tunachosubiri tu ni fedha zitakapotoka tutaainisha maeneo mbalimbali na tutazingatia Jimbo la Singida Mashariki. Ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Sita Mungaa ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kipindi cha Kampeni mwaka 2020 alipopita Jimbo la Singida Mashariki?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini ukiangalia majibu yake yanasema kwamba bado wanafanya tathmini ina maana hawajaanza na robo tayari ya mwaka tumeshapita.

Sasa swali langu ni lini watakwenda kujenga shule hizo ili watoto wa kike wasiweze kupata adha hizo kwa sababu tumeona adha wanazozipata watoto wa kike hasa Mkoa wa Iringa wanapata changamotoo kubwa sana. Kwa hiyo, tunaomba majibu ni lini wanaanza, tumeshapitisha robo sasa? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba robo ya kwanza ya mwaka imepita na bado inaonesha kama hatujafanya tathmini, kwa hiyo anachotaka kujua exactly ni lini? Ni kwamba Serikali ina mipango na mikakati yake na mimi nimwambie tu kwamba kabisa Serikali ya Awamu ya Sita hatutashindwa kukamilisha haya majengo kwa wakati. Moja ambacho hafahamu tunapojenga kwa mfano darasa ni muda wa miezi mitatu darasa linakuwa limekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunachokisubiri sasa hivi tu baada ya robo ya kwanza na mifumo ya fedha kufunguka kinachofuatia baada ya hapo ni fedha kuanza kuzitenga na kuzipeleka katika maeneo husika yaliyopangwa katika bajeti. Kwa hiyo, ninyi ondoeni wasiwasi Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan hii kazi tunaiweza na tutaimaliza kwa wakati. Ahsante. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Sita Mungaa ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kipindi cha Kampeni mwaka 2020 alipopita Jimbo la Singida Mashariki?

Supplementary Question 3

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi nilitaka niulize swali. Serikali ilikuwa na programu ya kukarabati shule kongwe nchi nzima ikiwepo Shule ya Sekondari Iringa Girls na Lugalo Secondary zilizopo Iringa ambazo ni za bweni kwa watoto wa kike na hasa watoto wenye ulemavu wa ngozi, viungo na wasioona. Pale hapakufanyika ukarabati wa mabweni mawili; moja katika shule ya Iringa Girls na nyingine Lugalo Secondary.

Je, ni lini sasa Serikali itatukamilishia mabweni yale ili watoto wale wenye ulemavu wasiendelee kupata shida ya mahali pa kulala? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri anazungumza kitu ambacho anakifahamu kwamba hizi shule alizozitaja ziko katika mipango yetu. Kwa hiyo, aondoe wasiwasi tu kwamba tutatekeleza ahadi ya kuwasaidia wanafunzi wote sio Iringa Girls na Lugalo ni shule zote kongwe tulizozikusudia zitafikiwa. Ahsante sana.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Sita Mungaa ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kipindi cha Kampeni mwaka 2020 alipopita Jimbo la Singida Mashariki?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ilishaahidi kujenga shule bora ya mfano ya wasichana katika kila mkoa nchini; na kwa kuwa shule hiyo ya mfano katika Mkoa wa Arusha tulikubaliana kwamba itajengwa katika Jimbo la Longido; na kwa kuwa tulishatenga eneo la kujengwa shule hiyo katika Kata ya Angekahang, ni lini ujenzi wa shule hiyo ya mfano kwa ajili ya wasichana wetu itaanza kujengwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mpaka sasa hivi tumeshaainisha maeneo yote 26 ambayo shule hizi zitajengwa baada ya kupata mapendekezo kutoka katika kila mkoa. Kwa hiyo, kinachosubiriwa sasa hivi tu ni fedha itoke na baada ya hapo tutapeleka fedha kwa awamu ya kwanza katika mikoa 10 ambayo tumeainisha mwaka huu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge atupe muda eneo lake halitabadilishwa na kazi hiyo itafanyika kama ambavyo imekusudiwa. Ahsante sana.