Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 95 2021-09-09

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Sita Mungaa ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kipindi cha Kampeni mwaka 2020 alipopita Jimbo la Singida Mashariki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa ujenzi wa shule 26 za wasichana, moja katika kila Mkoa na ujenzi wa shule 1,000 za sekondari kwenye kata zisizo na shule za sekondari ili kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na vikwazo hususani kwa watoto wa kike kutembea umbali mrefu. Vilevile, Serikali itafanya upanuzi wa shule za sekondari 100 kuweza kupokea wanafunzi zaidi wa kidato cha tano na sita.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa shule zote mpya za sekondari na upanuzi wa sekondari za kidato cha tano utafanyika kwa awamu. Awamu ya kwanza ya ujenzi itaanza mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 220. Kabla ya kuanza ujenzi, Serikali itafanya tathmini ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari na mahitaji ya upanuzi wa sekondari za kidato cha tano na sita ikiwa ni pamoja na Shule ya Sekondari Mungaa.