Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kurekebisha vifungashio vya mafuta ya mawese kwa kuwa wananchi wanaumizwa na kunyonywa kupitia vifungashio vinavyotumika sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru kwanza kwa majibu ya Serikali juu ya zao letu hili la mchikichi ambalo linazaa mafuta ya mawese. Kwa kweli mchikichi ni zao la kipekee sana Kitaifa na Kimataifa, na sisi pia tunategemea tukiona zao hili likiweza kuwanufaisha wananchi wa Kigoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 19 Desemba, 2020 Mheshimiwa Waziri Mkuu alikaa na wadau wa zao hili pale Kigoma ndani ya Ukumbi wa NSSF. Mojawapo ya mambo watu hawa waliomwambia wanahitaji kuona yakifanyiwa kazi ni Bodi ya Mawese na vifungashio maalum.

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Makanika.

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua sasa ni nini mkakati wa Serikali ulipofikia katika kutekeleza mambo haya ambayo walimwomba Waziri Mkuu yafanyiwe kazi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Assa Nelson Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, moja ya mikakati ambayo tunatekeleza ni kuanza sasa kutatua changamoto hizo, lakini zaidi tumeshaunda timu ya wataalam baada ya maelekezo ya Waziri Mkuu, wakati huo tumeshaunda timu ya wataalam kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara na Kilimo ambao sasa wataandaa guidelines kwa ajili ya vifungashio kwenye mazao haya ya kilimo na bidhaa zake, mazao yote ikiwemo ya mawese.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili la bodi, nadhani hili tunalichukua kama moja ya vitu vya kufanyia kazi kama Serikali ili tuweze kuona kama kuwepo kwa Bodi ya Michikichi ni moja ya suluhisho, basi nalo tutalifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kurekebisha vifungashio vya mafuta ya mawese kwa kuwa wananchi wanaumizwa na kunyonywa kupitia vifungashio vinavyotumika sasa?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Changamoto ya vifungashio ambayo ipo kwenye mawese ni sawasawa na changamoto ambayo ipo kwenye zao la viazi kule Makete, Mbeya na sehemu nyingine na Serikali ilituahidi.

Je, ni lini vifungashio rasmi vya viazi vitapatikana kwa wananchi wa Makete, Mkoa wa Njombe, Mbeya na sehemu nyingine ili tuondokane na changamoto ya lumbesa ambayo imekuwa ikisumbua kwa muda mrefu hadi sasa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema hiyo timu ambayo tumeiunda tumeshawapa deadline, kama ambavyo pia umesema, ndani ya mwezi mmoja waje na mkakati au mpango ambao utaweza kutatua changamoto hii. Kama nilivyosema, si kwa zao moja tu la viazi au michikichi na mazao mengine yote. Kwa sababu changamoto ya lumbesa iko katika mazao mengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lumbesa ni tatizo pale ambapo inazidi vipimo ambavyo vimekubalika katika zao husika. Kwa mfano katika hali ya kawaida tunasema gunia moja liwe kati ya kilo 95 mpaka 105, kwa hiyo zaidi ya hapo inakuwa ni shida. Sasa inaweza kuwa kifungashio ni kidogo kiasi kwamba ikaonekana kama ni lumbesa lakini kiko ndani ya uzito unaokubalika. Hata hivyo, tunachukua changamoto hizi, kama nilivyosema, Kamati hii itakwenda kuweka sasa mkakati au guidelines maalum kwa ajili ya kupata vifungashio specific kwa mazao maalum likiwemo hili la viazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.